Skip to main content

RC HOMERA AANIKA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera akielezea fursa za Uwekezaji zilizopo katika Mkoa huo wakati wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Katavi, Hafla inayofanyika katika Ukumbi wa Mpanda, Leo tarehe 3 Machi 2021.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Katavi, Hafla inayofanyika katika Ukumbi wa Mpanda, Leo tarehe 3 Machi 2021.

Wawekezaji  waliohudhuria uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji mkoani katavi wametakiwa kuchangamkia fursa za uwekezaji katika mkoa huo wenye zaidi ya hekta 45,000.

Akizungumza katika mkutano huo uliowakutanisha wadau wa uwekeaji kutoka maeneo mbalimbali, Mkuu wa mkoa huo Mhe Juma Homera amesema katika ujenzi wa viwanda mkoa umetenga hekari 245 kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda mbalimbali.

“Kutokana na wingi wa samaki wanaovuliwa kutoka ziwa Tanganyika wakiwemo, migebuka, kuhe, sangara pamoja na kamongo, mkoa umetenga hekari 245 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kusindika na kuchakata  samaki” Amekakaririwa Homera

Homera ameongeza kuwa wawekezaji wanayo fursa ya ujenzi wa viwanda mbalimbali vikiwemo viwanda vya usindikaji nafaka, ujenzi wa viwanda vya asali, uchakataji wa nyama na maziwa, pamoja na viwanda vya mbao.

Katika sekta ya utalii Homera amesema wawekezaji wanayofursa ya kuwekeza katika upande wa makampuni ya utalii yatakayosaidia ongezeko la utalii katika mkoa huo, wenye vivutio vingi va utalii ikiwemo mto mapacha ,mto maji moto pamoja na hifadhi ya taifa katavi yenye ukubwa wa hekari 4471.

“Tuna zaidi ya sokwe 2500, tuna tweiga mweupe ambae huwezi kumpata kokote Tanzania isipokuwa mkoani katavi, lakini pia tunao viboko  na tembo wakubwa sana kama nyumba” Amesema

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja