Skip to main content

RC HOMERA AANIKA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera akielezea fursa za Uwekezaji zilizopo katika Mkoa huo wakati wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Katavi, Hafla inayofanyika katika Ukumbi wa Mpanda, Leo tarehe 3 Machi 2021.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Katavi, Hafla inayofanyika katika Ukumbi wa Mpanda, Leo tarehe 3 Machi 2021.

Wawekezaji  waliohudhuria uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji mkoani katavi wametakiwa kuchangamkia fursa za uwekezaji katika mkoa huo wenye zaidi ya hekta 45,000.

Akizungumza katika mkutano huo uliowakutanisha wadau wa uwekeaji kutoka maeneo mbalimbali, Mkuu wa mkoa huo Mhe Juma Homera amesema katika ujenzi wa viwanda mkoa umetenga hekari 245 kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda mbalimbali.

“Kutokana na wingi wa samaki wanaovuliwa kutoka ziwa Tanganyika wakiwemo, migebuka, kuhe, sangara pamoja na kamongo, mkoa umetenga hekari 245 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kusindika na kuchakata  samaki” Amekakaririwa Homera

Homera ameongeza kuwa wawekezaji wanayo fursa ya ujenzi wa viwanda mbalimbali vikiwemo viwanda vya usindikaji nafaka, ujenzi wa viwanda vya asali, uchakataji wa nyama na maziwa, pamoja na viwanda vya mbao.

Katika sekta ya utalii Homera amesema wawekezaji wanayofursa ya kuwekeza katika upande wa makampuni ya utalii yatakayosaidia ongezeko la utalii katika mkoa huo, wenye vivutio vingi va utalii ikiwemo mto mapacha ,mto maji moto pamoja na hifadhi ya taifa katavi yenye ukubwa wa hekari 4471.

“Tuna zaidi ya sokwe 2500, tuna tweiga mweupe ambae huwezi kumpata kokote Tanzania isipokuwa mkoani katavi, lakini pia tunao viboko  na tembo wakubwa sana kama nyumba” Amesema

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...