Skip to main content

KAMA KUNA AKILI YA UWEKEZAJI BASI IKO KATAVI- PROF MKUMBO

Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera wakionyesha vitabu vya Uwekezaji mara baada ya kuzindua Muongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Katavi, Leo tarehe 3 Machi 2021.

Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Muongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Katavi, Leo tarehe 3 Machi 2021.
Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Muongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Katavi, Leo tarehe 3 Machi 2021.

Watumishi wa umma popote walipo nchini wametakiwa  moja ya kazi zao za msingi  iwe ni kuwawezesha na kuwasaidia watu na makampuni yanayotaka kuwekeza kufanya shuhuli zao bila bugudha yoyote.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo Mkoani Katavi  katika mkutano wa  uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji mkoani humo uliowakutanisha wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali.

“Kila siku tunasisitiza, mtumishi wa Umma ukitaka serikali ikuhudumie vizuri, lazima uwaheshimu na kuwathamini wawekezaji na yeyote anaye wanyanyasa na kuwadharau wawekezaji basi hajitambui” Amekaririwa Prof Mkumbo

Aidha, Prof Mkumbo amewataka wananchi kuondoa dhana ya kuwa uwekezaji ni suala linalofanywa na wageni tu, badala yake amewataka watu binafsi  na makampuni binafsi na hata wanafunzi wa vyuo vikuu  kujitokeza  kwa kuwa na mtaji, kufanyabiashara na kupata faida.

Muwekezaji sio lazima awe ni mtu tajiri sana au kutoka nje ya nchi, La hasha, hata wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali wana uwezo wa kuwa wawekezaji kwa kuweka akiba kutoka kwenye fedha zao za kujikimu na mwisho wa masomo anaweza akawa muwekezaji mkubwa” Amesisitiza

Hata hivyo Prof. Mkumbo pia amewataka wawekezaji kutimiza majukumu yao ya msingi ikiwa ni pamoja na kuwapa stahiki zao ikiwemo mikataba kwa wafanyakazi wao pamoja na  kushiriki kujitoa katika huduma za kijamii.

MWISHO

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...