Skip to main content

KAMA KUNA AKILI YA UWEKEZAJI BASI IKO KATAVI- PROF MKUMBO

Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera wakionyesha vitabu vya Uwekezaji mara baada ya kuzindua Muongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Katavi, Leo tarehe 3 Machi 2021.

Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Muongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Katavi, Leo tarehe 3 Machi 2021.
Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Muongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Katavi, Leo tarehe 3 Machi 2021.

Watumishi wa umma popote walipo nchini wametakiwa  moja ya kazi zao za msingi  iwe ni kuwawezesha na kuwasaidia watu na makampuni yanayotaka kuwekeza kufanya shuhuli zao bila bugudha yoyote.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo Mkoani Katavi  katika mkutano wa  uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji mkoani humo uliowakutanisha wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali.

“Kila siku tunasisitiza, mtumishi wa Umma ukitaka serikali ikuhudumie vizuri, lazima uwaheshimu na kuwathamini wawekezaji na yeyote anaye wanyanyasa na kuwadharau wawekezaji basi hajitambui” Amekaririwa Prof Mkumbo

Aidha, Prof Mkumbo amewataka wananchi kuondoa dhana ya kuwa uwekezaji ni suala linalofanywa na wageni tu, badala yake amewataka watu binafsi  na makampuni binafsi na hata wanafunzi wa vyuo vikuu  kujitokeza  kwa kuwa na mtaji, kufanyabiashara na kupata faida.

Muwekezaji sio lazima awe ni mtu tajiri sana au kutoka nje ya nchi, La hasha, hata wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali wana uwezo wa kuwa wawekezaji kwa kuweka akiba kutoka kwenye fedha zao za kujikimu na mwisho wa masomo anaweza akawa muwekezaji mkubwa” Amesisitiza

Hata hivyo Prof. Mkumbo pia amewataka wawekezaji kutimiza majukumu yao ya msingi ikiwa ni pamoja na kuwapa stahiki zao ikiwemo mikataba kwa wafanyakazi wao pamoja na  kushiriki kujitoa katika huduma za kijamii.

MWISHO

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja