Skip to main content

JESHI LA POLISI KATAVI LAMKAMATA MGANGA WA KIENYEJI KWA KUTOROSHA MWANAFUNZI

Na Swaum Katambo, Katavi

Jeshi la Polisi Mkoani Katavi limemkamata Mayala Hinyali (34) ambaye ni mganga wa kienyeji Mkazi wa Kasekese Wilayani Tanganyika kwa kumtorosha mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Usevya kidato cha kwanza jina limehifadhiwa na kwenda kuishi nae kinyumba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Benjamin Kuzaga amethibitisha hayo wakati akizungumza na kituo cha Habari Site Tv na kusema kuwa mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na atafikishwa mahakani kwa hatua zaidi za kisheria.

Kadhalika, Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi limefanikiwa kukamata mtandao wa watuhumiwa wanaojihusisha na wizi wa pikipiki ambapo Katika msako jeshi la polisi limefanikiwa kukamata jumla ya pikipiki kumi na mbili (12) na watuhumiwa kumi na watano.

Hata hivyo, Kamanda Kuzaga amesema Watuhumiwa hao pamoja na vielelezo vya pikipiki hizo zipo katika kituo cha polisi Mpanda, Huku watuhumiwa wakiendelea kuhojiwa na mara baada ya upelelezi kukamilika majalada hayo yatafikishwa katika ofisi ya Taifa mashitaka mkoa wa Katavi kwa hatua zaidi za kishiria.

Kamanda Kuzaga ametoa mwito kwa wananchi hasa kwa wale walioibiwa pikipiki kufika katika kituo cha Polisi Mpanda wakiwa na viambata vinavyotambulisha pikipiki zao ili kuweza kuzitambua.

Pia, amewataka wananchi kuwa karibu kwa namna ya kushirikiana katika kutoa ushahidi mahakamani hatua stahiki za kisheria kuchukuliwa ili kuweza kutokomeza kabisa wimbi  la wahalifu katika Mkoa wa Katavi.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja