Skip to main content

JESHI LA POLISI KATAVI LAMKAMATA MGANGA WA KIENYEJI KWA KUTOROSHA MWANAFUNZI

Na Swaum Katambo, Katavi

Jeshi la Polisi Mkoani Katavi limemkamata Mayala Hinyali (34) ambaye ni mganga wa kienyeji Mkazi wa Kasekese Wilayani Tanganyika kwa kumtorosha mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Usevya kidato cha kwanza jina limehifadhiwa na kwenda kuishi nae kinyumba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Benjamin Kuzaga amethibitisha hayo wakati akizungumza na kituo cha Habari Site Tv na kusema kuwa mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na atafikishwa mahakani kwa hatua zaidi za kisheria.

Kadhalika, Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi limefanikiwa kukamata mtandao wa watuhumiwa wanaojihusisha na wizi wa pikipiki ambapo Katika msako jeshi la polisi limefanikiwa kukamata jumla ya pikipiki kumi na mbili (12) na watuhumiwa kumi na watano.

Hata hivyo, Kamanda Kuzaga amesema Watuhumiwa hao pamoja na vielelezo vya pikipiki hizo zipo katika kituo cha polisi Mpanda, Huku watuhumiwa wakiendelea kuhojiwa na mara baada ya upelelezi kukamilika majalada hayo yatafikishwa katika ofisi ya Taifa mashitaka mkoa wa Katavi kwa hatua zaidi za kishiria.

Kamanda Kuzaga ametoa mwito kwa wananchi hasa kwa wale walioibiwa pikipiki kufika katika kituo cha Polisi Mpanda wakiwa na viambata vinavyotambulisha pikipiki zao ili kuweza kuzitambua.

Pia, amewataka wananchi kuwa karibu kwa namna ya kushirikiana katika kutoa ushahidi mahakamani hatua stahiki za kisheria kuchukuliwa ili kuweza kutokomeza kabisa wimbi  la wahalifu katika Mkoa wa Katavi.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...