Skip to main content

BENKI ZATAKIWA KUPUNGUZA URASIMU UTOAJI MIKOPO KWA WAWEKEZAJI



Na Swaumu Katambo, Katavi

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Abdallah Malela amewaomba watoa mitaji wa huduma za Kibenki  kuondoa tabia za Urasimu wa kuwachelewesha kuwapatia mitaji wawekezaji kwani inakwamisha maendeleo ya Nchi.

Ameyasema hayo leo Machi 5, 2020 ofisini kwake wakati akizungumza na Kituo cha Matangazo cha Site Tv kuhusu Matarajio ya Mkoa baada ya kufanyika uzinduzi wa Mwongozo wa Fursa za Uwekezaji Katavi uliofanyika Machi 3, 2020 katika Ukumbi wa Manispaa ya Mpanda.

Hata hivyo, Malela amesema kuwa uzinduzi umekuwa na manufaa makubwa kwani wawekezaji 17 walijitokeza siku hiyo huku akiwakaribisha wawekezaji wengine kuendelea kujitokeza kuwekeza katika Mkoa wa Katavi kwa kuwa maeneo bado yapo na fursa nyingi za Uchumi zinapatikana.

Kutokana na malalamiko ya wananchi wengi kuhitaji kitabu hicho cha Mwongozo wa Fursa za Uwekezaji Katavi kupatikana katika lugha ya Kiswahili Malela amesema kuwa Uongozi wa Mkoa wa Katavi una mpango wa kuandaa makala pamoja na nakala zitakazoandikwa kwa lugha za Kiswahili, Kifaransa, Kiarabu n.k

MWISHO

Comments

  1. M/MUNGU AZIDI KUWABARIKI WANA KATAVI NA VIONGOZI WAO WOTE WA KATAVI WAZIDI KUWA NA MOYO WA KUSAIDIA NA KULETA MAENDELEO KATAVI NA KWA TANZANIA KWA UJUMLA.. KATAVI OYEEEE.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja