Skip to main content

BENKI ZATAKIWA KUPUNGUZA URASIMU UTOAJI MIKOPO KWA WAWEKEZAJI



Na Swaumu Katambo, Katavi

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Abdallah Malela amewaomba watoa mitaji wa huduma za Kibenki  kuondoa tabia za Urasimu wa kuwachelewesha kuwapatia mitaji wawekezaji kwani inakwamisha maendeleo ya Nchi.

Ameyasema hayo leo Machi 5, 2020 ofisini kwake wakati akizungumza na Kituo cha Matangazo cha Site Tv kuhusu Matarajio ya Mkoa baada ya kufanyika uzinduzi wa Mwongozo wa Fursa za Uwekezaji Katavi uliofanyika Machi 3, 2020 katika Ukumbi wa Manispaa ya Mpanda.

Hata hivyo, Malela amesema kuwa uzinduzi umekuwa na manufaa makubwa kwani wawekezaji 17 walijitokeza siku hiyo huku akiwakaribisha wawekezaji wengine kuendelea kujitokeza kuwekeza katika Mkoa wa Katavi kwa kuwa maeneo bado yapo na fursa nyingi za Uchumi zinapatikana.

Kutokana na malalamiko ya wananchi wengi kuhitaji kitabu hicho cha Mwongozo wa Fursa za Uwekezaji Katavi kupatikana katika lugha ya Kiswahili Malela amesema kuwa Uongozi wa Mkoa wa Katavi una mpango wa kuandaa makala pamoja na nakala zitakazoandikwa kwa lugha za Kiswahili, Kifaransa, Kiarabu n.k

MWISHO

Comments

  1. M/MUNGU AZIDI KUWABARIKI WANA KATAVI NA VIONGOZI WAO WOTE WA KATAVI WAZIDI KUWA NA MOYO WA KUSAIDIA NA KULETA MAENDELEO KATAVI NA KWA TANZANIA KWA UJUMLA.. KATAVI OYEEEE.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...