Skip to main content

WATOTO 8,000 MKOANI RUVUMA KUFAIDIKA NA MAFUNZO YA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

SHIRIKA lisilokuwa la kiserikali la kuhudumia watu wasiojiweza na wenye Ulemavu (PADI) linatarajia kuanza kutoa mafunzo ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa watoto wa kiume wenye umri wa miaka tisa hadi 14 katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Meneja Mradi wa PADI Gifti Kilasi amesema kupitia mradi wa USAID KIZAZI KIPYA unnaoratibiwa na PADI,utaanza kutoa mafunzo kwa watoto hao ili waweze kufahamu madhara ya ukatili wa kijinsia na waanze kupinga ukatili huo katika jamii.

Kwa mujibu wa Meneja huyo, Mradi huo umeanza kutekelezwa mwaka 2017 na unatarajia kukamilika mwaka 2021 na kwamba hadi sasa wamesajili watoto 900 wa shule za Msingi na lengo ni kuwafikia watoto 8000 katika Mkoa wa Ruvuma hadi kufikia Septemba 2021.

Ameongeza kuwa wamegeukia kundi hilo kwa sababu ni wahanga wa ukatili wa kijinsi,na kwamba kundi hilo lilisahaulika katika kuwapa elimu ya kupambana na ukatili wa kijinsia ukilinganisha na watoto wa kike.

Afisa Ustawi wa Halmashauri ya Wilaya ya songea Suzana Mkondya amewaasa wazazi na walezi kutoa taarifa pale watoto wa kiume wanapofanyiwa vitendo vya ukatili katika jamii. 

Amesema baada ya mafunzo hayo wanatarajia matendo vitendo vya ukatili vitapungua kwa kiasi kikubwa na watoto wataelimika na kuanza kutoa elimu kwa vijana wengine.

Hata hivyo amesema mafunzo hayo yatatolewa kwa nadharia na vitendo kupitia michezo na kwamba yatafundishwa na walimu wa shule za msingi katika maeneo husika na watoto watapata fursa ya kupima afya zao bure.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Zena Ibrahimu ametoa wito kwa wadau wa mradi huo kusimamia vizuri na kutoa ushirikiano wa dhati katika utekelezaji wa mradi huo ili uweze kutoa matokeo chanya ya kujenga na kulinda maadili mema ya kitanzania.

Ibrahimu amewataja Watoto watakaofaidika na mafunzo hayo wanatoka katika Kata za Parangu, Maposeni, Kilagano, Litapwasi, Mpitimbi,Kizuka,Litisha,Magagula,Peramiho na Mbinga mhalule na kwamba kila kata zimechaguliwa shule tatu na kila shule wamechaguliwa wanafunzi 30.

Imeandikwa na Jakline Clavery

Afisa Habari Halmashauri ya Wilaya ya Songea

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...