Skip to main content

WAFUGAJI SONGEA WAASWA KUSAJILIWA NA KUTAMBULIKA KISHERIA

baadhi ya wafugaji katika kijiji cha Nambendo Halmashauri ya Wilaya ya Songea wakimsikiliza Afisa Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri yan Wilaya ya Songea Dr.Erick Kahise

Na Jacqelen Clavery -Afisa Habari

Songea DC

WAFUGAJI Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wametakiwa kujisajili na kutambulikakisheria katika maeneo wanayoishi ili serikali iweze kuwahudumia kulingana mahitaji yao.

Afisa Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri hiyo Dr.Erick Kahise ametoa wito huo wakati alipokutana na kufanya kikao na wafugaji katika cha Kijiji cha Nambendo kata ya Ndongosi.

Dr.Kahise amesema usajili wa mifugo utawezesha serikali kutoa huduma stahiki kwa wafugaji kufuatia takwimu sahihi zilizotolewa na wafugaji wenyewe waliopo katika eneo husika.

Dr.Kahise amesema takwimu zitasaidia pia kutenga maeneo ya malisho,ujenzi wa majosho,dawa za uchanjaji wa mifugo,uwekaji wa miundo mbinu na huduma nyingine za kiutalam.

Dkt Kahise ameyataja magonjwa 14 ya kipaumbele ambayo serikali inataka wafugaji kutilia mkazo katika swala zima la chanjo kwa Wanyama wote wanaofugwa.

Amewaagiza wafugaji hao kutokiuka Sheria namba 17 ya mwaka 2003 inayosimamia mifugo kufuata taratibu za kuchanja mifugo kwa sababu chanjo inaboresha afya ya mifugo na kwamba mifugo ikiimarika na uchumi wao pia utaimarika na serikali itakusanya maduhuri,sanjari na kuimarisha lishe katika familia.

“kwa mwaka chanjo itatolewa mara mbili,na bei za chanjo hizo ni bei elekezi ya serikali ambayo haizidi shilingi.1000,na adhabu ya kutochanja mifugo inafikia hadi shilingi 20,000’’,alisema.

Afisa Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Wilaya ya Songea Dr.Erick Kahise akizungumza na wafugaji kuhusu usajiri wa mifugo na sheria za ufugaji katika kijiji cha Nambendo\

Naye mwenyekiti wa Kijiji cha Nambendo Shaibu Rashidi Makomba amesema mpaka Septemba 15 ,2020 wamesajili wafugaji 17 kati ya wafugaji 115.

Amesema idadi ndogo ya wafugaji waliojitokeza kujisajiri inasababishwa na udanganyifu unaofanywa na wafugaji hao kuficha ukweli kuhusu idadi kamili ya mifugo wanayo miliki.

Ametoa rai kwa wafugaji na wakulima katika Kijiji hicho kushirikiana katika shughuli za maendeleo na kuacha tabia ya kuendekeza migogoro isiyokuwa na tija kwao.

Halmashauri ya wilaya ya Songea imetenga maeneo ya machungio katika kata za Muhukuru Lilihi,Muhukuru barabarani na Ndongosi.

 

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja