Skip to main content

WAFUGAJI SONGEA WAASWA KUSAJILIWA NA KUTAMBULIKA KISHERIA

baadhi ya wafugaji katika kijiji cha Nambendo Halmashauri ya Wilaya ya Songea wakimsikiliza Afisa Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri yan Wilaya ya Songea Dr.Erick Kahise

Na Jacqelen Clavery -Afisa Habari

Songea DC

WAFUGAJI Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wametakiwa kujisajili na kutambulikakisheria katika maeneo wanayoishi ili serikali iweze kuwahudumia kulingana mahitaji yao.

Afisa Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri hiyo Dr.Erick Kahise ametoa wito huo wakati alipokutana na kufanya kikao na wafugaji katika cha Kijiji cha Nambendo kata ya Ndongosi.

Dr.Kahise amesema usajili wa mifugo utawezesha serikali kutoa huduma stahiki kwa wafugaji kufuatia takwimu sahihi zilizotolewa na wafugaji wenyewe waliopo katika eneo husika.

Dr.Kahise amesema takwimu zitasaidia pia kutenga maeneo ya malisho,ujenzi wa majosho,dawa za uchanjaji wa mifugo,uwekaji wa miundo mbinu na huduma nyingine za kiutalam.

Dkt Kahise ameyataja magonjwa 14 ya kipaumbele ambayo serikali inataka wafugaji kutilia mkazo katika swala zima la chanjo kwa Wanyama wote wanaofugwa.

Amewaagiza wafugaji hao kutokiuka Sheria namba 17 ya mwaka 2003 inayosimamia mifugo kufuata taratibu za kuchanja mifugo kwa sababu chanjo inaboresha afya ya mifugo na kwamba mifugo ikiimarika na uchumi wao pia utaimarika na serikali itakusanya maduhuri,sanjari na kuimarisha lishe katika familia.

“kwa mwaka chanjo itatolewa mara mbili,na bei za chanjo hizo ni bei elekezi ya serikali ambayo haizidi shilingi.1000,na adhabu ya kutochanja mifugo inafikia hadi shilingi 20,000’’,alisema.

Afisa Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Wilaya ya Songea Dr.Erick Kahise akizungumza na wafugaji kuhusu usajiri wa mifugo na sheria za ufugaji katika kijiji cha Nambendo\

Naye mwenyekiti wa Kijiji cha Nambendo Shaibu Rashidi Makomba amesema mpaka Septemba 15 ,2020 wamesajili wafugaji 17 kati ya wafugaji 115.

Amesema idadi ndogo ya wafugaji waliojitokeza kujisajiri inasababishwa na udanganyifu unaofanywa na wafugaji hao kuficha ukweli kuhusu idadi kamili ya mifugo wanayo miliki.

Ametoa rai kwa wafugaji na wakulima katika Kijiji hicho kushirikiana katika shughuli za maendeleo na kuacha tabia ya kuendekeza migogoro isiyokuwa na tija kwao.

Halmashauri ya wilaya ya Songea imetenga maeneo ya machungio katika kata za Muhukuru Lilihi,Muhukuru barabarani na Ndongosi.

 

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...