Skip to main content

RC HOMERA:PENGINE NYASI ZIMEOTA KWENYE MIILI YAO,SIO KWENYE UWANJA WA NDEGE

 

Na Mwandishi wetu Site Tv

Mpanda-Katavi

MKUU wa Mkoa wa Katavi Juma Zuberi Homera ametibuka nyongo baada ya Watu aliodai ni waongo kusambaza taarifa za kuwa Uwanja wa Ndege Mpanda Mkoani humo umejaa Nyasi haufanyi kazi.

Akizungumza na Site Tv leo Septemba 17 alipowasili uwanjani hapo kuwapokea Watalii,Homera amekanusha taarifa hizo huku akiwajibu wanaosema hivyo kuwa ni wapotoshaji na hawakuwahi kufika katika Uwanja huo kujionea hali halisi.

"Hawa wanaosema uwanja huu umeota nyasi,nionyeshe masikitiko yangu pengine nyasi zimeota kwenye Miili yao au kwenye Mwili wake. Na Sisi tuko tayari Wananchi wa Katavi kwenda kufyeka hizo Nyasi kwenye Mwili wa huyo Mtu ambaye ameongopa mchana kweupe na Watu wakiwa wanashuhudia"-RC Homera,Katavi.
Baadhi ya abiria kwenye Uwanja wa Ndege Mpanda wakielekea kupanda Ndege kwa ajili ya Safari 

Aidha,Homera amesema hivi sasa katika uwanja huo vimefungwa vifaa vya kisasa ambavyo vitaziwezesha Ndege kutua muda wowote hata kama ni msimu wa Mvua.

Kwa upande wake Meneja wa Uwanja wa Ndege Mpanda Ndg. Jeff Shantiwa amesema kwa sasa Abiria wapo wa kutosha na Ndege inajaa,na amesisitiza kuwa Ulinzi na Usalama katika uwanja huo ni wa kutosha.
Jeff Shantiwa,Meneja Uwanja wa Ndege Mpanda

Kumekuwa na maneno kwenye mitandao ya Kijamii kuwa Ndege zinazofanya safari Mkoani humo hazijai huku wengine wakidai safari zipo mara Moja tu kwa Wiki badala ya mara Tatu kwa Wiki yaani Jumamosi,Jumanne na Alhamisi.
Ndege(Air Tanzania) ikiwa imetua katika uwanja wa Ndege Mpanda Mkoani Katavi

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...