Skip to main content

RC HOMERA:PENGINE NYASI ZIMEOTA KWENYE MIILI YAO,SIO KWENYE UWANJA WA NDEGE

 

Na Mwandishi wetu Site Tv

Mpanda-Katavi

MKUU wa Mkoa wa Katavi Juma Zuberi Homera ametibuka nyongo baada ya Watu aliodai ni waongo kusambaza taarifa za kuwa Uwanja wa Ndege Mpanda Mkoani humo umejaa Nyasi haufanyi kazi.

Akizungumza na Site Tv leo Septemba 17 alipowasili uwanjani hapo kuwapokea Watalii,Homera amekanusha taarifa hizo huku akiwajibu wanaosema hivyo kuwa ni wapotoshaji na hawakuwahi kufika katika Uwanja huo kujionea hali halisi.

"Hawa wanaosema uwanja huu umeota nyasi,nionyeshe masikitiko yangu pengine nyasi zimeota kwenye Miili yao au kwenye Mwili wake. Na Sisi tuko tayari Wananchi wa Katavi kwenda kufyeka hizo Nyasi kwenye Mwili wa huyo Mtu ambaye ameongopa mchana kweupe na Watu wakiwa wanashuhudia"-RC Homera,Katavi.
Baadhi ya abiria kwenye Uwanja wa Ndege Mpanda wakielekea kupanda Ndege kwa ajili ya Safari 

Aidha,Homera amesema hivi sasa katika uwanja huo vimefungwa vifaa vya kisasa ambavyo vitaziwezesha Ndege kutua muda wowote hata kama ni msimu wa Mvua.

Kwa upande wake Meneja wa Uwanja wa Ndege Mpanda Ndg. Jeff Shantiwa amesema kwa sasa Abiria wapo wa kutosha na Ndege inajaa,na amesisitiza kuwa Ulinzi na Usalama katika uwanja huo ni wa kutosha.
Jeff Shantiwa,Meneja Uwanja wa Ndege Mpanda

Kumekuwa na maneno kwenye mitandao ya Kijamii kuwa Ndege zinazofanya safari Mkoani humo hazijai huku wengine wakidai safari zipo mara Moja tu kwa Wiki badala ya mara Tatu kwa Wiki yaani Jumamosi,Jumanne na Alhamisi.
Ndege(Air Tanzania) ikiwa imetua katika uwanja wa Ndege Mpanda Mkoani Katavi

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja