Skip to main content

WAZIRI Mkuchika amwakilisha Rais Magufuli ufunguzi ofisi ya TAKUKURU Namtumbo

 

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu Gorge Mkuchika amemwakilisha Rais Magufuli katika ufunguzi wa jengo la ofisi ya TAKUKURU Wilaya ya Namtumbo lililogharimu zaidi ya shilingi milioni 139.

Akizungumza kabla ya kufungua jengo hilo katika hafla iliyofanyika mjini Namtumbo Waziri Mkuchika amesema Rais Dkt.John Magufuli amemteua kufungua jengo hilo kwa niaba yake na kwamba Rais ameweka utaratibu wa kuyafungua majengo mapya ya TAKUKURU kwa nyakati tofauti na wasaidizi wake.

Ameagiza majengo mapya saba ya TAKUKURU ngazi ya wilaya yatumike vema katika mapambano dhidi ya rushwa pamoja na kuwafichua wala rushwa sanjari na kuacha kushiriki katika vitendo vya rushwa.

“Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Jemedari Rais wetu,imefanya kazi kubwa ya kuimarisha na kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi nchini’’,alisisitiza Waziri Mkuchika.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt.Mstaafu Gorge Mkuchika akifungua ofisi ya TAKUKURU Namtumbo

Kwa mujibu wa Waziri Mkuchika,ripoti ya Benki ya Dunia ya Septemba 26,2019,imeeleza kuwa Tanzania imeongoza kwa kupunguza umaskini miongoni mwa nchi za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara.

Kulingana na Waziri Mkuchika,ripoti nyingine ya Benki ya Dunia inayoitwa Human Capital,The Real Wealth Of Nationals iliyotoka Julai 2019 ilionesha kuwa umasikini nchini Tanzania umepungua kutoka asilimia 34.4 hadi kufikia asilimia 26.8.

Waziri Mkuchika amesema ufanisi wa jitihada za serikali katika mapambano dhidi ya rushwa nchini katika mwaka 2018/2019 zimeendelea kuonesha pia kupitia taarifa za utafiti wa kupima hali ya rushwa duniani unaofanywa na wadau wa mapambano dhidi ya rushwa na utawala bora kama Taasisi ya Transparency International, MO Ibrahim na Afro Barometer.

“Taarifa za Taasisi hizo zote kwa miaka mitatu kuanzia mwaka 2016 hadi 2018 zinaonesha kuwa Tanzania imeendelea kufanya vyema katika mapambano dhidi ya Rushwa’’,alisisitiza Mkuchika. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU aliyewakilishwa na Mkurugenzi wa Uzuiaji Rushwa wa TAKUKURU Sabina Seja amesema jengo hilo ni moja kati ya majengo mapya saba ya TAKUKURU ngazi ya Wilaya yaliojengwa kwa wakati mmoja.

Ofisi mpya ya TAKUKURU wilaya ya Namtumbo iliyogharimu zaidi ya shilingi milioni 139

Seja amesema TAKUKURU katika Mkoa wa Ruvuma hadi kufikia Juni 2020 imefanikiwa kuchunguza ubadhirifu na kuokoa kiasi cha fedha zaidi ya shilingi milioni 740.

‘Fedha hizo zimeweza kuokolewa kutokana na uchunguzi katika Benki ya wananchi wa Mbinga,vyama vya ushirika na kuwezesha baadhi ya watuhumiwa kurejesha fedha,vitendo hivyo vya ubadhirifu vilikuwa vinadumaza maendeleo ya ushirika nchini’’,alisema Seja.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme akizungumza katika hafla hiyo amewaasa TAKUKURU kuendelea kuwang’ata wala rushwa na mafisadi wote bila kuwaonea na kuwapendelea ili kutomekeza rushwa nchini.

Mndeme amesema jengo hilo la TAKUKURU wilaya ya Namtumbo litaimarisha utendaji kazi wa watumishi wa TAKUKURU na kurahisisha watoa taarifa na mashahidi watakaoletwa katika opereshani mbalimbali za mapambano ya rushwa na kufanya kazi kwa uhuru na usiri zaidi.

Imeandikwa na Albano Midelo 

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Namtumbo

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...