Skip to main content

Wakulima Ruvuma watakiwa kuchangamkia fursa ya kilimo bora cha kahawa

Uzalishaji wa Kahawa Mbinga

Wakulima wa Mkoa wa RUVUMA wametakiwa kuchangamkia fursa ya miche ya kilimo bora cha kahawa kwa sababu maeneo mengi ndani ya Mkoa yanafaa kwa kilimo cha kahawa ambacho kitainua uchumi wao.

Wito huo umetolewa na mtaalam wa kilimo Bw Victa Akulumuka kutoka kituo cha utafiti wa zao la kahawa TaCRI cha Ugano Mbinga katika maonesho ya nanenane ngazi ya Mkoa wa Ruvuma yanayofanyika viwanja wa Msamala mjini Songea.

Akalumuka amesema wakulima wanatakiwa kuchangamkia fursa ya kulima zao la kahawa kwakuwa zao la kahawa linaonekana kustawi katika maeneo mengi ndani ya mkoa na kilimo ambacho kitainua uchumumi wao na Taifa.

Amewataka wakulima kuzingatia amri kumi za kilimo cha kahawa ambazo zinasaidia katika kustawisha zao la kahawa ambazo zitatoa matokeo chanya na kuongeza uzalishaji wenye tija kwa wakulima .

Amezitaja amri za kilimo bora cha kahawa kuwa ni kukatia matawi,kutumia mbolea,kupulizia madawa kwa wakati,kupalilia nakuondoa machipukizi Pamoja na kupanda miti kwa ajili ya kutunza ubaridi katika shamba.

Shamba la Kahawa la AVIV Kipokela

Aidha amesema endapo wakulima watafuatilia na kusimamia na kufuatilia kilimo cha kahawa mkulima anaweza kuvuna kilo tatu kwa shina moja,ambapo kwa hekali moja mkulima anaweza kuvuna kilo Zaidi ya 1500 kutokana na shamba lenye ukubwa wa hekali moja ambapo hupandwa miche 540

Ameomba maafisa ugani wa wa Halmashauri mkoani Ruvuma kutoa elimu juu ya usimamizi na ufuatiliaji wa zao la kahawa kwalengo la kuwasaidia wakulima kupata mavuno mengi na kunufaika na kilimo cha kahawa ambacho ni miongoni mwa mazao ya kimkakati Nchini.

“Ukichukulia miaka 10 iliyopita eneo la Liganga wilayani Songea kwenye shamba la kahawa la AVIV palikuwa hapajulikani kama panafaa kulima zao la kahawa lakini kampuni ya AVIV imeonesha mfano kwamba ardhi ya Ruvuma inafaa kwa kilimo cha kahawa”,alisema Akalumuka.

Utafiti umebaini kuwa mkoa wa Ruvuma una maeneo mengi ambayo yanafaa kwa kilimo cha zao la kahawa ikiwemo Wilaya Mbinga na wilaya ya Songea katika kata za Liganga,Mbingamhalule,Kizuka,Parangu LItisha,Ndongosi na Mpitimbi na Madaba.

Kituo cha utafiti wa zao la kahawa TaCRI kinatoa huduma ya miche bure kwa wakulima wote na utaalama wa kulima zao la kahawa unapatika kutoka kwa maafisa ugani.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...