Skip to main content

TCRA YAOMBA HALMASHAURI NCHINI KUTUMIA FURSA ZA KUFUNGUA ANUNI ZA MAKAZI.




Na Mwandishi Wetu.Katavi.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeziomba Halmashauri zote nchini kutumia fursa za kufungua anuani za makazi (Post Code) ili kuboresha maisha ya wananchi kupitia huduma za mawasiliano.
Kauli hiyo imetolewa hapo jana kwenye semina ya siku moja katika ukumbi wa Idara ya maji Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi na Mhadisi wa Mamlaka hiyo kanda za Nyanda za Juu Kusini,Charles Thomas alipokuwa akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Mkoani humo.
Mhandisi Charles aliziomba halmashauri kuwa kitendo cha  kufunguliwa wa anuani za makazi kwenye halmashauri zitachochea ukuaji katika sekta ya mawailiano nchini ikiwa pamoja kutumia fursa  za tehema hasa mkongo wa taifa wa mawasiliano kwa maendeleo.


Akifafanua umuhimu wa anuani za makazi kwa Halmashauri Mhadisi huyo alibainisha kuwa zitaweza kusadia katika ukusanyaji wa mapato yatokanayo na kodi kwa wananchi kwani watakuwa na takwimu halisia za anuani za makazi ya watu wanapoishi au biashara zao wanapo fanyia  hivyo kusaidia kuwafikia kwa haraka.
Vilevile kusaidia katika mazoezi mbalimbali ya kitaifa kama vile undikishwaji wananchi yaani sensa,kuongeza utalii,kufanya  tafiti, pamoja na undikishwaji wa mali kama vile nyumba,biashara,wapiga kura.
"...mwaka 2002 kwenye zoezi la mwisho kufanyika la sensa kuna baadhi ya maeneo ilikuwa ni ngumu kufika kwa sababu ya kutokujua welekeo halisi wa makazi ya watu "Alisema Mhadisi Charles.
Pamoja na hayo Halmashauri zimeombwa kuomba mafunzo maalumu kutoka mamla ya mawasiliano nchini mafunzo ambayo  yatawaongeza uwezo kwa  maafisa wa Halmashauri katika kutekeleza zoezi zima la ufunguaji wa anuani za makazi.
Katika hatua nyingine Afsa masoko wa TCRA Nyanda za Juu kusini Elias Joseph aliweka wazi kuwa mamlaka hiyo wajibu wake ni kuweka mazingira sawa ya utendaji kazi ili kuimarisha ushindani wa haki na kukuza maendeleo ya kiuchumi.
Aidha alibainisha kuwa ni kulinda masirahi ya wateja kama vile watumiaji wa mitandao mbalimbali ya simu ikiwa pamoja na kusimamia rasilimali masafa na namba zinazotumika katika utoaji wa  huduma za mawasiliano ya simu.
Joseph alisema kuwa  kwa kuzigatia shughuri za TCRA kuwa za kisasa kwa kutumia teknolojia sahihi katika kuimarisha tafiti zenye ubora wa huduma zinazodhibitiwa ,uwezo,na umahiri wa watumiaji.
Vilevile aliwapa tahadhari kubwa wananchi  kuepuka kununua simu kiholela bali wazingatie kununua kwenye maduka ambayo yamesajili kwenye mamlaka hayo huku wakihakikisha wanadai list za malipo pindi wanaponunua simu zao.


Kwa upande wa kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Tanganyika Gwamaka Owden wakifunga semina hiyo licha ya kuishukuru TCRA Nyanda za Juu kusini alisema kuwa zoezi la kuazisha anuani za makazi kwa wananchi watalitekeleza haraka iwezekanavyo ambapi litawasaidia katika upangaji mji.
Oweden aliiambia TCRA kuwa hawatasita kuchua hatua yoyote ikiwame ya kuomba mafunzo maalumu kutoka mamlaka hiy0 pindi itakapohitajika katika kuboresha ufanisi wa utengenezaji wa anuani za makazi.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja