Skip to main content

RC KATAVI AWASWEKA MAHABUSU VIONGOZI GRAND TOBACCO NA KASOKOLA AMCOS,ACHARUKA HADI PESA ZILIPWE









Na Swaum Katambo,Site News

Mpanda,Katavi.

Kufuatia maagizo ya siku 10 aliyowahi kuyatoa katika kikao cha wadau wa uoteshaji wa Miti Katavi kuhusu Kampuni za PETROBENA na GRAND TOBACCO kuwalipa Fedha wakulima wa Tumbaku Mkuu wa Mkoa Juma Homera leo Aug 3 ameamuru kuwekwa mahabusu Viongozi wa Kampuni ya GRAND TOBACCO kwa kudaiwa zaidi ya Dola Laki 3 kwa zaidi ya Mwezi mzima.

"Nimeamuru Viongozi hawa wawekwe Mahabusu mpaka walipe hizo fedha,na hivi nnavyozungumza wameshapelekwa Mahabusu na wanaendelea kuhojiwa na vyombo vya sheria kuhakikisha kwamba fedha hizo hawatatoka ndani Mpaka walipe Fedha za wakulima ambazo zinatakiwa zilipwe baada ya kuchukua Tumbaku ya Wakulima".Alisema Mh Homera

Kwa upande Wa Kampuni ya PETROBENA yenyewe imelipa  Dola Laki moja na Elfu 40 huku wakidaiwa zaidi ya Dola Elfu 40 na Kampuni ya GRAND TOBACCO yenyewe haikulipa Kabisa huku Mh Juma Homera akisisitiza kutowaachia hadi pesa hizo zitakapoliwa.

Kwa upande mwingine Mh.Homera alisema kuwa kuna wananchi watano ambao bado hawajalipwa Fedha zao na Kasokola Amcos toka mwaka 2018 hadi hivi sasa wanaendelea kuzungushwa huku Amcos hiyo ikiwa na tuhuma za kuingiza majina hewa na kuuza Tumbaku kwa njia zisizo halali na kuacha Madeni kwenye Chama hicho cha Msingi hivyo madeni hayo kuhamishiwa kwa wakulima

"Tumeamua hao na bodi yao yote wawekwe Mahabusu mpaka walipwe hao wakulima watano ili tuweze kuhakikisha kwamba wananchi wanafurahia serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Dkt.John Pombe Magufuli kwamba inatenda haki kwa wananchi" .Alisema

Kuhusu mustakabali wa wakulima Mh Homera amesema kuwa mpaka hivi sasa Kampuni ya PREMIUM  watanunua Tumbaku iliyobakia ambayo ilikuwa imesalia bado haijanunulika mpaka hivi sasa.

"Watanunua Tanganyika Amcos,Ilela Amcos na Mishamo Amcos baada ya mazungumzo na TTB (Bodi ya Tumbaku Tanzania) maana yake ni kwamba makampuni yaliyojiondoa kwenye kununua Tumbaku ya awamu ya pili yatanunuliwa na Kampuni nyingine". Aliongeza Mh.Homera

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...