Skip to main content

RC KATAVI APONGEZA WAKULIMA WALIOJITOKEZA KWENYE MAONYESHO YA NANENANE JIJINI MBEYA,ASISITIZA NA UTALII

 

Na Mwandishi wetu,Site Tv

Nanenane-Mbeya

#NEWS Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Zuberi Homera ameridhishwa na bidhaa za Wafanyabiashara kutoka Mkoani Katavi,baada ya kutembelea mabanda yao katika maonyesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yanayoendelea viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya.


Homera akiwa ameambatana na Viongozi wengine akiwemo Katibu Tawala wa Mkoa Ndugu Abdalah Malela,Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda,Mh. Salehe Mhando wa Tanganyika na Jamilla Kimaro wa Mpanda baada ya kutembelea baadhi ya Mabanda amesema.

"Nimefarijika na namna maandalizi yalivyofanyika,kiukweli Mkoa wa Katavi wamejipanga vizuri,nimeona kwenye mabanda yao yanaridhisha,yanaendana na kauli mbiu ya Mheshimu Rais wetu Tanzania ya Viwanda,unaweza kuona wametengeneza Wine nzuri, wametengeneza unga mzuri, wametengeneza asali vizuri,na wana Viwanda vya asali kwa mfano ukienda kule Bulamata na maeneo mengine"-Alisema RC Homera, alipotembelea mabanda ya Nanenane.

"Lakini Manispaa nao wametengeneza bidhaa nzuri sana,kama vile neti n.k,hii inaonyesha kwamba Wananchi wamebadilika,na ndiyo maana siku zote nasisitiza lazima tuwe na siku ya Masoko ya ndani katika Mkoa wetu wa Katavi. Lazima tuwe na Siku 2 au Tatu za Masoko ya ndani,kwahiyo tutaainisha ni sehemu gani nzuri kwaajili ya kuuza bidhaa zetu katika Mkoa wa Katavi ili maisha yaweze kuendelea"-RC Homera,katika Viwanja vya Maonyesho ya Nanenane Jijini Mbeya.


Akiwa katika banda la Ofisi za Shirika la Hifadhi la Taifa Tanzania (TANAPA),Mh Homera ameshauri kuwepo na utaratibu wa upatikaji Nyama za Wanyama Pori ili kukata kiu ya Watanzania wanaopenda nyama hiyo.

"Mtu mpaka anazaliwa na anakufa hajawahi kula nyama ya Swala,sasa ni changamoto kubwa,Mimi nawashauri tu kwamba TAWA ndo mnazile WMA n.k,wekeni utaratibu ili nyama ziweze kupatikana,Watu wana hamu za nyama pori. Jambo lingine nyama ya Pori ni dawa,Mnyama pori anakula majani,majani yale yana virutubisho mbalimbali,akila na yeye anapata virutubisho,ndiyo maana Wazee wetu waliishi Miaka mingi kwa sababu walikula sana nyama za pori.-"RC Homera

Aidha,amewakaribisha Watanzania wote kwenda kutalii na kutembelea vivutio vilivyopo Mkoani Katavi ikiwemo Mto Mapacha,Twiga Mweupe,Viboko na Mamba.
-
"Mkoa wa Katavi kama mnavyofahamu tunavyo vivutio vikubwa vya utalii,ukitika Katavi ndiyo unakutana na Twiga Mweupe,ukifika Katavi unakutana na Viboko zaidi ya Elfu Kumi,na ndiyo hifadhi yenye Viboko wengi Tanzania"RC Homera,Katika Maonyesho ya NaneNane Jijini Mbeya

"Lakini pia utakutana na Mamba,Mamba watulivu lakini wakali,ukifika Katavi utakutana na Maji ya Mto Mapacha,ukipata yale Maji unauwezo wa kuzaa Mapacha,zaidi ya Kaya 30 mpaka sasahivi tunavyozungumza,zilikuwa Kaya 28 na zinazidi kuongezeka wanazaa Mapacha,kwahiyo Ndugu Waaandishi wa Habari Mimi nawakaribisha sana"-Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Zuberi Homera

"Kama unahitaji Watoto mpigo mpigo,basi unaweza ukaja ukapata Maji ya Mto Mapacha ukanywa Wewe na Mpenzi wako mkazaa Mapacha,na wale Watoto Mapacha sio misukule,ni Watoto halisi kabisa kwasababu wapo na wanaakili timamu kabisa,na yale Maji ni mazuri kabisa."-Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Zuberi Homera.


#SiteNews
#TukutaneSite
#TukutaneKazini

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...