Skip to main content

PETROLI KATAVI YAGEUKA LULU,NAULI BAJAJI BODABODA ZAPANDA KAWA KASI





Na Swaum Katambo,Site News

Mpanda,Katavi

Hali ya upatikanaji wa Mafuta ya Petroli Manispaa ya Mpanda sio shwari kutokana na kuadimika kwa Mafuta hayo huku wafanyabiashara  waendesha vyombo vya moto ikiwemo bajaji na pikipiki wakilalamika kuomba utatuzi wa changamoto hiyo.

Mafuta ya Petroli Manispaa ya Mpanda yanapatikana katika kituo kimoja tuu cha Kampuni ya SERENIVA kilichopo Kata ya Majengo Manispaa hii  huku Meneja wa Kituo hicho Thomas Magabe amesema kuwa shida ya mafuta imetokana na wauzaji kutoa Mafuta kidogo huku wakilazimika kutoa oda mapema kwenye visima vya matuta.


Baadhi ya wafanyabiashara vyombo vya Moto wakiwa kwenye kituo cha Mafuta SERENIVA

Nao wafanyabiashara wa vyombo vya moto hususan bajaji na pikipiki ambao ndio waathirika zaidi wamesema  wanatumia muda mwingi kwenye foleni  huku ikiwagharimu kibiashara na kupelekea hadi kupandisha bei ya kawaida  ya usafiri iliyozoeleka.

Kwa upande wake Amani Mahela Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara na Mhasibu wa Kamati ya baraza la ushauri la Mkoa linalosimamia bidhaa zinazodhibitiwa na EWURA,amesema hali hiyo ya ufinyu wa mafuta imetokana na baadhi ya changamoto za usafiri kutokea njiani ikiwemo magari yanayosafirisha mafuta hayo kuharibika njiani huku akisema hadi ifikapo kesho August 4 tatizo hilo litakwisha

Ingia Youtube kujionea hali ilivyokuwa
https://youtu.be/2qjPzV4-mU8

#SiteNews
#TukutaneSite
#TukutaneKazini

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja