Skip to main content

PETROLI KATAVI YAGEUKA LULU,NAULI BAJAJI BODABODA ZAPANDA KAWA KASI





Na Swaum Katambo,Site News

Mpanda,Katavi

Hali ya upatikanaji wa Mafuta ya Petroli Manispaa ya Mpanda sio shwari kutokana na kuadimika kwa Mafuta hayo huku wafanyabiashara  waendesha vyombo vya moto ikiwemo bajaji na pikipiki wakilalamika kuomba utatuzi wa changamoto hiyo.

Mafuta ya Petroli Manispaa ya Mpanda yanapatikana katika kituo kimoja tuu cha Kampuni ya SERENIVA kilichopo Kata ya Majengo Manispaa hii  huku Meneja wa Kituo hicho Thomas Magabe amesema kuwa shida ya mafuta imetokana na wauzaji kutoa Mafuta kidogo huku wakilazimika kutoa oda mapema kwenye visima vya matuta.


Baadhi ya wafanyabiashara vyombo vya Moto wakiwa kwenye kituo cha Mafuta SERENIVA

Nao wafanyabiashara wa vyombo vya moto hususan bajaji na pikipiki ambao ndio waathirika zaidi wamesema  wanatumia muda mwingi kwenye foleni  huku ikiwagharimu kibiashara na kupelekea hadi kupandisha bei ya kawaida  ya usafiri iliyozoeleka.

Kwa upande wake Amani Mahela Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara na Mhasibu wa Kamati ya baraza la ushauri la Mkoa linalosimamia bidhaa zinazodhibitiwa na EWURA,amesema hali hiyo ya ufinyu wa mafuta imetokana na baadhi ya changamoto za usafiri kutokea njiani ikiwemo magari yanayosafirisha mafuta hayo kuharibika njiani huku akisema hadi ifikapo kesho August 4 tatizo hilo litakwisha

Ingia Youtube kujionea hali ilivyokuwa
https://youtu.be/2qjPzV4-mU8

#SiteNews
#TukutaneSite
#TukutaneKazini

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...