Skip to main content

Msitafute migogoro na vyama vya siasa

Aliyesimama ni msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Songea mjini akifungua mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata Manispaa ya Songea

MSIMAMIZI wa Uchaguzi Jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma Tina Sekambo amewatahadharisha wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata katika Manispaa hiyo kuepuka migogoro na vyama vya siasa kwa kwa kusimamia mchakato wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria za Tume ya Uchaguzi.

Sekambo ametoa tahadhari hiyo kwenye ukumbi wa Manispaa hiyo mjini Songea, wakati anazungumza kabla ya kufungua mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wasaidizi kutoka kata zote 21 kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu.

“Tume ya Uchaguzi inasisitiza sana,tusitafute migogoro na vyama vya siasa,tuepuke kabisa migogoro ,uchaguzi asilimia 100 unaendeshwa na sheria ,ukikosea hata nukta ni tatizo,tunatakiwa tusome maelekezo yote vizuri ili kufanya mchakato wa uchaguzi mwaka huu kwa ufanisi’’,alisisitiza Sekambo.

Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Songea mjini Tina Sekambo akifungua mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata katika jimbo hilo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea

Msimamizi huyo wa Uchaguzi Jimbo la Songea mjini pia amewataka wasimamizi hao wasaidizi siku ya wagombea kuchukua fomu hadi siku ya uteuzi wanatakiwa kuwepo ofisini muda wote na kwamba siku tatu kabla, wanasiasa wanaruhusiwa kuleta fomu zao na kukaguliwa kubaini iwapo zina makosa au zipo sahihi.

Amesema Tume ya uchaguzi imeamua kutoa mafunzo hayo ya siku tatu ili kufanikisha zoezi la Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ambapo amewaasa kuhakikisha wanazingatia mafunzo yote ambayo watapewa na Tume ya Uchaguzi badala ya kufanyakazi kwa mazoea.

“Hakikisheni mnazingatia matakwa ya Katiba,Sheria,Kanuni zinazosimamia Uchaguzi,maadili ya uchaguzi na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na NEC’’,alisisitiza Sekambo.

Kwa upande wake Afisa Uchaguzi Manispaa ya Songea Christopher Ngonyani amesema mafunzo hayo yameshirikisha wasimamizi wasaidizi 42 kutoka Kata 21 zilizopo katika Manispaa hiyo na kwamba wote walioteuliwa na NEC wamehudhuria mafunzo hayo.

Afisa Uchaguzi huyo amewaasa washiriki wa mafunzo kuzingatia mafunzo wanayopewa na kuhakikisha kila msimamizi anayatambua maeneo ambayo atafanyia kazi ikiwemo miundombinu ya kufika katika kata na vituo vya kupigia kura.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya wasimamzi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata Manispaa ya Songea wakipata mafunzo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea yanayotolewa na Tume ya  Uchaguzi (1)

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata katika Manispaa ya Songea wameapishwa na Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi mkoani Ruvuma Livini Lyakinana.

Uchaguzi Mkuu wa Rais,wabunge na madiwani unatarajia kufanyika nchini Oktoba 28 mwaka huu.

Imeandikwa na Albano Midelo 

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja