Skip to main content

Msitafute migogoro na vyama vya siasa

Aliyesimama ni msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Songea mjini akifungua mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata Manispaa ya Songea

MSIMAMIZI wa Uchaguzi Jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma Tina Sekambo amewatahadharisha wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata katika Manispaa hiyo kuepuka migogoro na vyama vya siasa kwa kwa kusimamia mchakato wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria za Tume ya Uchaguzi.

Sekambo ametoa tahadhari hiyo kwenye ukumbi wa Manispaa hiyo mjini Songea, wakati anazungumza kabla ya kufungua mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wasaidizi kutoka kata zote 21 kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu.

“Tume ya Uchaguzi inasisitiza sana,tusitafute migogoro na vyama vya siasa,tuepuke kabisa migogoro ,uchaguzi asilimia 100 unaendeshwa na sheria ,ukikosea hata nukta ni tatizo,tunatakiwa tusome maelekezo yote vizuri ili kufanya mchakato wa uchaguzi mwaka huu kwa ufanisi’’,alisisitiza Sekambo.

Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Songea mjini Tina Sekambo akifungua mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata katika jimbo hilo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea

Msimamizi huyo wa Uchaguzi Jimbo la Songea mjini pia amewataka wasimamizi hao wasaidizi siku ya wagombea kuchukua fomu hadi siku ya uteuzi wanatakiwa kuwepo ofisini muda wote na kwamba siku tatu kabla, wanasiasa wanaruhusiwa kuleta fomu zao na kukaguliwa kubaini iwapo zina makosa au zipo sahihi.

Amesema Tume ya uchaguzi imeamua kutoa mafunzo hayo ya siku tatu ili kufanikisha zoezi la Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ambapo amewaasa kuhakikisha wanazingatia mafunzo yote ambayo watapewa na Tume ya Uchaguzi badala ya kufanyakazi kwa mazoea.

“Hakikisheni mnazingatia matakwa ya Katiba,Sheria,Kanuni zinazosimamia Uchaguzi,maadili ya uchaguzi na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na NEC’’,alisisitiza Sekambo.

Kwa upande wake Afisa Uchaguzi Manispaa ya Songea Christopher Ngonyani amesema mafunzo hayo yameshirikisha wasimamizi wasaidizi 42 kutoka Kata 21 zilizopo katika Manispaa hiyo na kwamba wote walioteuliwa na NEC wamehudhuria mafunzo hayo.

Afisa Uchaguzi huyo amewaasa washiriki wa mafunzo kuzingatia mafunzo wanayopewa na kuhakikisha kila msimamizi anayatambua maeneo ambayo atafanyia kazi ikiwemo miundombinu ya kufika katika kata na vituo vya kupigia kura.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya wasimamzi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata Manispaa ya Songea wakipata mafunzo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea yanayotolewa na Tume ya  Uchaguzi (1)

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata katika Manispaa ya Songea wameapishwa na Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi mkoani Ruvuma Livini Lyakinana.

Uchaguzi Mkuu wa Rais,wabunge na madiwani unatarajia kufanyika nchini Oktoba 28 mwaka huu.

Imeandikwa na Albano Midelo 

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...