Skip to main content

ETC AGRO TRACTOR NA CRDB KUKUZA KILIMO CHENYE TIJA KATAVI.





Na Mwandishi Wetu,
      Katavi.

Wakulima Mkoa wa Katavi wameombwa kuachana na kilimo cha mazoea ambacho hakimkomboi  mkulima kiuchumi na badala yake kumfanya kuzalisha mazao ya chakula na biashara yasiyokuwa na tija huku yakimwacha masikini.

Kauli hiyo imetolewa jana kwenye ukumbi wa Idara ya Maji Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi na Afsa Masoko na Mauzo wa ETC Agro Tractor,Zahra Salum wakati akizungumza na wadau wa kilimo mkoani humo ambapo aliwaambia kuwa kilimo pekee chenye tija kitamkomboa mkulima kutoka kwenye umasikini.

Zahra aliweka wazi kuwa kwa kutambua juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya rais Dkt John Magufuli ya kuadaa sera madhubuti za kuhakikisha sekta ya kilimo inakua kwa kasi na kumfanya mkulima kupiga hatua za maendeleo ya kiuchumi ndio zimeifanya Kampuni ya ETC Agro Tractor kwa kushirikiana na Benki ya CRDB Tawi la Mpanda kuandaa mfumo ambao utamfanya mkulima kupata zana za kilimo za kisasa,




Mfumo huo ambao umewekwa na ETC Agro Tractor ni kumpatia mkulima matrekta kwa bei nafuu sambamba na kuigia ubia na Benki ya CRDB ambapo mkulima ataweza kukopeswa bila masharti ili wakulima wadowadogo  waweze kunufaika.

“…mikopo hii ya matrekta kulingana na mkataba tuliofanya na CRDBank mkulima hatakiwi kutoa dhamana ya aina yoyote bali dhamana yake itakuwa ni trekta hilohilo ambalo anapokabidhiwa,Kadi ya trekta itabaki benki kwa muda wa miaka mitatu hadi pale mkulima atakapomaliza kulipa deni ndipo atakabidhiwa na kumiliki mojakwa moja”Alisisitiza Afsa masoko huyo.



Vilevile Zahra alisema kuwa mikopo ya matrekta inakuwa nafuu kwa sababu wakulima watapaswa kufanya marejesho ya malipo ya fedha mara moja kwa kila mwaka,kulipia kiasi cha fedha asilimia 35 ya thamani ya trekta pamoja na mkulima kuwa na hekali 20 za kwake binafsi au za kukodi kwa mkataba kwani ndizo zitambulisha mwananchi kama ni mkulima na kuepuka watu walanguzi.

Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Mpanda Hamand Masoud alisema kuwa mkoa wa Katavi kwa sasa unapaswa kupiga hatua kubwa kwenye sekta ya kilimo ili mkulima aweze kunufaika kwa kuzalisha mazao yenye tija.

Masoud alisema hatua ambazo mkoa unapaswa kuchukua ni pamoja na wakulima kuachana na zana duni za kilimo kama vile majembe ya mkono au yakukokotwa na n’gombe.




Aidha Meneja huyo alifafanua kuwa Mkoa wa Katavi umebarikiwa kuwa na mvua za kutosha na ardhi yenye rutuba,Hivyo wakulima wanapaswa kuchangamkia fursa hizo za kutumia zana za kilimo za kisasa ili mkoa uweze kuongoza kitaifa kwenye uzalishaji wa mazao ya chakula ikiwa na mkulima kukuza uchumi wake binafsi na taifa kwa ujumla.

Gabriel Simon Mkazi wa Kijiji cha Mwese Wilaya ya Tanganyika Mkoa humo akizungumza kwa niamba ua wakulima alipongeza Taasisi za Kibeki pamoja na makampuni yanayosaidia wakulima kujikwamua kiuchumi.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...