Skip to main content

DC KIMARO AWATAKA WADAU WA ELIMU NSIMBO KUFANYIA KAZI KWA VITENDO MAADHIMIO

 

Na John Alex Mganga

Nsimbo -Katumba.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh.Bi Jamila Kimaro amewataka Wadau wa Elimu Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kuyafanyia kazi kwa vitendo maazimio mbalimbali  yaliyotolewa katika kikao hicho ili kuinua ubora wa Elimu Nsimbo.

Mh.Kimaro ametoa rai hiyo wakati akifunga kikao cha wadau wa Elimu Nsimbo  Kilichofanyika Agosti 18 ,2020  katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Katumba kwa lengo la kujadili changamoto mbalimbali na kuzipatia ufumbuzi ili kuinua Ubora wa Elimu ndani ya Halmashauri ya Nsimbo

Kudumisha Ushirikiano baina ya Walimu na Wazazi katika kuhakikisha kuwa changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Elimu ikiwemo utoaji wa chakula inapatiwa ufumbuzi,Uzingatiaji utoaji wa Elimu ya Awali,Uboreshaji wa miundombinu pamoja na kuzingatia utekelezaji wa maazimio yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Cde.Juma Zuberi Homera ni maazimio yaliyoazimiwa na Wadau wa Elimu Nsimbo katika kikao hicho.

Akizungumza  ukumbini hapo Mh.Kimaro mesema ni muhimu kwa Wadau walioshiriki katika Kikao hicho Nsimbo  kuyachukua maazimio yatokanayo na kikao hicho na kuyapeleka mpaka ngazi ya Kijiji  ili kuwapa fursa Wananchi kushiriki katika kutekeleza kwa Vitendo yale yaliyoazimiwa jambo litakalosaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto mbalimbali zinazoikumba Sekta ya Elimu Nsimbo.

Mh.Jamila ametoa wito kwa Wadau wa Elimu kuhakikisha kuwa wanakomesha tabia ya kuwatumikisha Wanafunzi katika shughuli binafsi za walimu ama za Wananchi na badala yake kuhakikisha kuwa Wanafunzi hao wanashiriki katika shughuli za Shule zikiwemo zile za Kilimo katika maeneo ya Shule yaliyotengwa ili kujihakikishia uwepo wa Chakula Mashuleni.

Amewataka Wazazi wa Wanafunzi Nsimbo kujitoa kwa moyo kuchangia Chakula Shuleni ili kuwawezesha watoto kupata chakula cha kutosha jambo litalaowawezesha watoto hao kuwa na Afya nzuri hali itakayowaezesha kufanya vizuri katika masomo yao na hivyo kuinua ubora wa Elimu Nsimbo.

Mh.Kimaro amepiga marufuku Wananchi Nsimbo kuwapangisha Wanafunzi hususani wa kike na badala yake washiriki kikamilifu katika kuchangia ujenzi wa Mabweni ya Wanafunzi hao ili kudhibiti vitendo mbalimbali vinavyoathiri  masomo  ikiwemo mimba kwa watoto wa kike sambamba na  kuwaepusha watoto wa kiume kujihusisha na utumiaji wa madawa ya kulenya.

Mkuu huyo wa Wilaya pia amewataka Wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Walimu ikiwa ni sambamba na kujenga mazingira mazuri yatayowezesha Walimu na Watumishi katika Sekta ya Elimu kupenda mazingira ya kazi jambo litakalosaidia kuinua ubora wa Elimu Nsimbo.

Pamoja na mambo mengine Mh.Jamila ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kwa jitihada mbalimbali zinazofanywa katika kuinua ubora wa Elimu ambapo amewataka Watendaji wa Halmashauri kuongeza juhudi zaidi ili kuhakikisha kuwa wanainua ubora wa Elimu Nsimbo.

Awali akizungumza kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Katavi  katika ufunguzi wa kikao cha wadau wa elimu Nsimbo Katibu Tawala Msaidizi Elimu Bi.Newaho Mkisi pamoja na pongezi amewataka Wadau wa Elmu kuhakikisha kuwa wanatekeleza kwa vitendo maazimio mbalmbali yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi kuinua ubora wa Elimu pamoja na yale yatakayoazimiwa ili kuinua ubora wa Elimu Nsimbo.

Wiki ya Wadau wa Elimu  imeanza rasmi Agosti 17 ambapo  Kilele chake kinatarajiwa kuadhimishwa  Wilayani Tanganyika mapema Agosti 21 mwaka huu ambapo Washindi mbalimbali waliofanya vizuri katika kuinua ubora wa Elimu ikiwemo Ufaulu zitatolewa siku hiyo.



Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja