Skip to main content

DC KIMARO AWATAKA WADAU WA ELIMU NSIMBO KUFANYIA KAZI KWA VITENDO MAADHIMIO

 

Na John Alex Mganga

Nsimbo -Katumba.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh.Bi Jamila Kimaro amewataka Wadau wa Elimu Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kuyafanyia kazi kwa vitendo maazimio mbalimbali  yaliyotolewa katika kikao hicho ili kuinua ubora wa Elimu Nsimbo.

Mh.Kimaro ametoa rai hiyo wakati akifunga kikao cha wadau wa Elimu Nsimbo  Kilichofanyika Agosti 18 ,2020  katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Katumba kwa lengo la kujadili changamoto mbalimbali na kuzipatia ufumbuzi ili kuinua Ubora wa Elimu ndani ya Halmashauri ya Nsimbo

Kudumisha Ushirikiano baina ya Walimu na Wazazi katika kuhakikisha kuwa changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Elimu ikiwemo utoaji wa chakula inapatiwa ufumbuzi,Uzingatiaji utoaji wa Elimu ya Awali,Uboreshaji wa miundombinu pamoja na kuzingatia utekelezaji wa maazimio yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Cde.Juma Zuberi Homera ni maazimio yaliyoazimiwa na Wadau wa Elimu Nsimbo katika kikao hicho.

Akizungumza  ukumbini hapo Mh.Kimaro mesema ni muhimu kwa Wadau walioshiriki katika Kikao hicho Nsimbo  kuyachukua maazimio yatokanayo na kikao hicho na kuyapeleka mpaka ngazi ya Kijiji  ili kuwapa fursa Wananchi kushiriki katika kutekeleza kwa Vitendo yale yaliyoazimiwa jambo litakalosaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto mbalimbali zinazoikumba Sekta ya Elimu Nsimbo.

Mh.Jamila ametoa wito kwa Wadau wa Elimu kuhakikisha kuwa wanakomesha tabia ya kuwatumikisha Wanafunzi katika shughuli binafsi za walimu ama za Wananchi na badala yake kuhakikisha kuwa Wanafunzi hao wanashiriki katika shughuli za Shule zikiwemo zile za Kilimo katika maeneo ya Shule yaliyotengwa ili kujihakikishia uwepo wa Chakula Mashuleni.

Amewataka Wazazi wa Wanafunzi Nsimbo kujitoa kwa moyo kuchangia Chakula Shuleni ili kuwawezesha watoto kupata chakula cha kutosha jambo litalaowawezesha watoto hao kuwa na Afya nzuri hali itakayowaezesha kufanya vizuri katika masomo yao na hivyo kuinua ubora wa Elimu Nsimbo.

Mh.Kimaro amepiga marufuku Wananchi Nsimbo kuwapangisha Wanafunzi hususani wa kike na badala yake washiriki kikamilifu katika kuchangia ujenzi wa Mabweni ya Wanafunzi hao ili kudhibiti vitendo mbalimbali vinavyoathiri  masomo  ikiwemo mimba kwa watoto wa kike sambamba na  kuwaepusha watoto wa kiume kujihusisha na utumiaji wa madawa ya kulenya.

Mkuu huyo wa Wilaya pia amewataka Wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Walimu ikiwa ni sambamba na kujenga mazingira mazuri yatayowezesha Walimu na Watumishi katika Sekta ya Elimu kupenda mazingira ya kazi jambo litakalosaidia kuinua ubora wa Elimu Nsimbo.

Pamoja na mambo mengine Mh.Jamila ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kwa jitihada mbalimbali zinazofanywa katika kuinua ubora wa Elimu ambapo amewataka Watendaji wa Halmashauri kuongeza juhudi zaidi ili kuhakikisha kuwa wanainua ubora wa Elimu Nsimbo.

Awali akizungumza kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Katavi  katika ufunguzi wa kikao cha wadau wa elimu Nsimbo Katibu Tawala Msaidizi Elimu Bi.Newaho Mkisi pamoja na pongezi amewataka Wadau wa Elmu kuhakikisha kuwa wanatekeleza kwa vitendo maazimio mbalmbali yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi kuinua ubora wa Elimu pamoja na yale yatakayoazimiwa ili kuinua ubora wa Elimu Nsimbo.

Wiki ya Wadau wa Elimu  imeanza rasmi Agosti 17 ambapo  Kilele chake kinatarajiwa kuadhimishwa  Wilayani Tanganyika mapema Agosti 21 mwaka huu ambapo Washindi mbalimbali waliofanya vizuri katika kuinua ubora wa Elimu ikiwemo Ufaulu zitatolewa siku hiyo.



Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...