Skip to main content

JESHI LA POLISI KATAVI LAPEWA MASAA 48 KUMPELEKA RAIA WA CHINA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUSHINDWA KUNAWA MIKONO



 
Mkuu wa Mkoa wa Katavi comrade Juma Homerawa kwanza kutoka kulia kwenye picha.


Na Mwandishi Wetu
       Katavi.

 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ametowa saa 48 kwa jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kumfikisha Mahakamani Raia wa Nchi ya China aitwaye  Lin  Guosong (34) mfabiashara Mkazi wa Mtaa wa Majengo Manispaa ya Sumbawanga ambae alikamatwa kwa tuhuma za  kukataa kutii mashariti ya kujikinga na ugonjwa wa Corona  COVID -19. 
 
 Homera alitowa maagizo hayo hapo  (leo) jana mbele ya wandishi wa habari mara baada ya kukabidhiwa vifaa tiba vya kujikinga na ugonjwa wa COVID -19.

 Vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 25 vilitolewa na  shirika la Walter Reed walivyokabidhi msaada kwa Mkuu wa Mkoa na Meneja wa mradi Walter Reed (HJFMRI) Dkt  Shaban  Ndama .

Alisema  Raia huyo wa Nchi ya China alikamatwa na jeshi la polisi katika eneo la Kijiji cha  Kasansa  Tarafa ya Mamba Wilayani Mlele Mkoani Katavi na kisha kupelekwa katika kituo cha polisi cha Majimoto baada ya kukataa kutii amri ya kujikinga na ugonjwa wa Corona kwa kukataa kunawa maji yenye dawa .

  Alieleza kuwa raia huyo wa nchi ya China alikamatwa katika  Kijiji cha Kasansa Tarafa ya Mamba Wilayani Mlele Mkoani hapa baada ya kukaidi agizo la  kukinga na kujiadhari na ugonjwa corona
.
 Raia huyo wa  china  siku hiyo akiwa kwenye kizuizi alitakiwa   na kamati maalumu ya  Mkoa kuna maji yenye dawa kwa ajiri ya kujiadhari na kujikinga na maambukizi ya corona .

 Pamoja na kutakiwa kutekeleza agizo hilo Raia huyo  wa China Lin  Guosong alikaidi hari ambayo ilifanya polisi wa mkamate  na kumfikisha katika kituo cha polisi cha maji moto .

  Alisema baada ya kuwa amekamatwa yeye Mkuu wa  Mkoa aliagiza   mtuhumiwa huyo  hati yake ichukuliwe na iwe chini ya jeshi la polisi .

 Mkuu wa Mkoa Homera aliagiza kuwa kutokana na kitendo hicho cha Raia wa China kukaidi amri halali ya Serikali ya Mkoa wa Katavi analiagiza jeshi la Polisi RPC   Mkoa wa katavi kuhakikisha ndani ya saa 48 wanamfikisha Mahakamani Raia huyo wa china ili akajibu tuhuma zinazomkabili .

 Alisisitiza kuwa Mkoa huu umejipanga kuhakikisha wanajikinga na ugonjwa wa corona hivyo mtu yoyote ambae atakaidi maagizo yaliyotolewa   atachukuliwa hatua bila kujari cheo cha mtu au rangi ya mtu .

 Amewaonya watu wanao ishi kwenye makazi ya wakimbizi ya Katumba na Mishamo waliokuwa raia ya nchi ya Burundi ambao wamepewa uraia wa nchi ya Tanzania kuacha tabia ya kuwapokea ndugu zao wanaotoka nchi ya Burundi  kwa kuingia nchini kwa kupitia njia ambazo sio rasmi kwani wanaweza kusababisha kuwepo kwa corona.

 Mganga  Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Omari  Sukari alisema mpaka sasa Mkoa wa  Katavi hauna mgonjwa hata mmoja alipatikana na maambukizi hayo ila wanawashikilia watu wanne waliowaweka kwenye karantini raia wa nchi ya DRC walioingia nchini kwa njia za panya kwa kupitia  mwambao wa ziwa Tanganyika.

Alisema  Mkoa huu wamejipanga kuhakikisha uonjwa huu hauingii kabisa katika Mkoa na kauli mbiu yao ya Mkoa ni Mkoa wa Katavi bila Corona covid 19 inawezekana .

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja