Skip to main content

JESHI LA POLISI KATAVI LAPEWA MASAA 48 KUMPELEKA RAIA WA CHINA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUSHINDWA KUNAWA MIKONO



 
Mkuu wa Mkoa wa Katavi comrade Juma Homerawa kwanza kutoka kulia kwenye picha.


Na Mwandishi Wetu
       Katavi.

 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ametowa saa 48 kwa jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kumfikisha Mahakamani Raia wa Nchi ya China aitwaye  Lin  Guosong (34) mfabiashara Mkazi wa Mtaa wa Majengo Manispaa ya Sumbawanga ambae alikamatwa kwa tuhuma za  kukataa kutii mashariti ya kujikinga na ugonjwa wa Corona  COVID -19. 
 
 Homera alitowa maagizo hayo hapo  (leo) jana mbele ya wandishi wa habari mara baada ya kukabidhiwa vifaa tiba vya kujikinga na ugonjwa wa COVID -19.

 Vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 25 vilitolewa na  shirika la Walter Reed walivyokabidhi msaada kwa Mkuu wa Mkoa na Meneja wa mradi Walter Reed (HJFMRI) Dkt  Shaban  Ndama .

Alisema  Raia huyo wa Nchi ya China alikamatwa na jeshi la polisi katika eneo la Kijiji cha  Kasansa  Tarafa ya Mamba Wilayani Mlele Mkoani Katavi na kisha kupelekwa katika kituo cha polisi cha Majimoto baada ya kukataa kutii amri ya kujikinga na ugonjwa wa Corona kwa kukataa kunawa maji yenye dawa .

  Alieleza kuwa raia huyo wa nchi ya China alikamatwa katika  Kijiji cha Kasansa Tarafa ya Mamba Wilayani Mlele Mkoani hapa baada ya kukaidi agizo la  kukinga na kujiadhari na ugonjwa corona
.
 Raia huyo wa  china  siku hiyo akiwa kwenye kizuizi alitakiwa   na kamati maalumu ya  Mkoa kuna maji yenye dawa kwa ajiri ya kujiadhari na kujikinga na maambukizi ya corona .

 Pamoja na kutakiwa kutekeleza agizo hilo Raia huyo  wa China Lin  Guosong alikaidi hari ambayo ilifanya polisi wa mkamate  na kumfikisha katika kituo cha polisi cha maji moto .

  Alisema baada ya kuwa amekamatwa yeye Mkuu wa  Mkoa aliagiza   mtuhumiwa huyo  hati yake ichukuliwe na iwe chini ya jeshi la polisi .

 Mkuu wa Mkoa Homera aliagiza kuwa kutokana na kitendo hicho cha Raia wa China kukaidi amri halali ya Serikali ya Mkoa wa Katavi analiagiza jeshi la Polisi RPC   Mkoa wa katavi kuhakikisha ndani ya saa 48 wanamfikisha Mahakamani Raia huyo wa china ili akajibu tuhuma zinazomkabili .

 Alisisitiza kuwa Mkoa huu umejipanga kuhakikisha wanajikinga na ugonjwa wa corona hivyo mtu yoyote ambae atakaidi maagizo yaliyotolewa   atachukuliwa hatua bila kujari cheo cha mtu au rangi ya mtu .

 Amewaonya watu wanao ishi kwenye makazi ya wakimbizi ya Katumba na Mishamo waliokuwa raia ya nchi ya Burundi ambao wamepewa uraia wa nchi ya Tanzania kuacha tabia ya kuwapokea ndugu zao wanaotoka nchi ya Burundi  kwa kuingia nchini kwa kupitia njia ambazo sio rasmi kwani wanaweza kusababisha kuwepo kwa corona.

 Mganga  Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Omari  Sukari alisema mpaka sasa Mkoa wa  Katavi hauna mgonjwa hata mmoja alipatikana na maambukizi hayo ila wanawashikilia watu wanne waliowaweka kwenye karantini raia wa nchi ya DRC walioingia nchini kwa njia za panya kwa kupitia  mwambao wa ziwa Tanganyika.

Alisema  Mkoa huu wamejipanga kuhakikisha uonjwa huu hauingii kabisa katika Mkoa na kauli mbiu yao ya Mkoa ni Mkoa wa Katavi bila Corona covid 19 inawezekana .

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...