Skip to main content

DC MHANDO ATANGAZA VITUO 58 VYA KUNUNULIA MAZAO YA NAFAKA TANGANYIKA.





 
Add captionMkuu wa Wilaya ya Tanganyika Saleh Mhando akizungumza na waadishi wa habari ofisini kwake kartika kijiji cha Ifukutwa akitaja jumla ya vituyo 58 vya kununulia mazao mbalimbali ikiwamo pia kuwahimiza wakulima kutumia mfumo wa stakabadhi gharani.



Na Mwandishi Wetu
      Tanganyika.

Wakulima wa mazao ya chakula na biashara wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi wameshauriwa kuuza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi gharani pamoja na maeneo ya vituo maalumu yaliyotengwa kibiashara na Wilaya hiyo ili kunufaika na uzalishaji wao.  

Akizungumza jana ofsini kwake katika Kata ya Ifukutwa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Saleh Mhando  aliweka wazi kuwa utaratibu wa mfumo wa stakabadhi gharani na kuweka vituo maalumu vya kibiashara (soko) wameamua kuanzisha ili kuhakikisha mkulima anaweza kunufaika.

Mhando aliainisha baadhi ya mazao ambayo yatatumika kuuzwa kupitia stakabadhi gharani ni Alzeti,Pamba,Kahawa,Korosho,Tumbaku na ufuta huku mazao ya 
Mahidi,Karanga,Mpunga,Mhongo,Mtama pamoja na viazi vitanunuliwa katika vituo maalumu vilivyowekwa na Wilaya hiyo.

Katika kuhakikisha ufanisi wa utaratibu huo uliowekwa unazingatiwa Mkuu wa wilaya hiyo alisema kuwa Mkulima yeyote yule hataruhusiwa kuuza mazao yake nje ya maeneo ya vituo vilivyotengwa sambamba na wanunuzi hawataruhusiwa kununua bila kuzingatia utaratibu huo.

“…utaratibu uliokuwa ukitumika hapo awali wa kumwita mfanyabiashara nyumbani au shambani na kupima mazao umeisha kuazia leo hii,Na yeyote atakaye bainika kufanya hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake”Alisisitiza Mhado.

Utaratibu mwingine utakao tumika ni mazao yote kuuzwa kwa kutumia mizani zilizozibitishwa na wakala wa vipimo ili kuepusha mkulima kuuibiwa mazao yake.Ikiwa pamoja na kupiga marufuku  utumiaji wa ndoo aina ya Mozambique ambazo husababisha hasara kwa mkulima.

Mkuu wa wilaya hiyo akitaja vituo vitakavyo tumika kununulia mzao hayo ni jumla ya kata zote za wilaya ya Tanganyika zitatumika na kuwa na jumla ya vituo 58 huku akisisitiza kuwa hapatakuwa na vituo zaidi ya viwili kwenye eneo moja bali kutakuwa na kituo kimoja ambacho wanunuzi wote watatumia kununulia mazao hayo.

Aidha alisema kuwa wafanyabiashara wote hawataweza kuruhusiwa kununua mazao bila kuwa na kibali cha biashara pamoja na kibali cha ununuzi kutoka ofisi ya Mkurugenzi huku kutakuwa na kibali maalumu cha kusafirishia mazao yaliyonunuliwa kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya isipokuwa kwa watu wale watakao kuwa wanasafirisha mazao chini ya tani moja.



 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika John Rumuri akiwa akizungumzia kanuni na taratibu za wakulima na wafanyabiashara katika utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi gharani hasa akiwahimiza wafanyabiashara kwenda ofsini kwake kwa ajili ya kujipatia vibali vya kununulia mazao



Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Tanganyika John Rumuri alisema kuwa kunafaida nyingi zaidi za kutumia mfumo wa stakabadhi gharani pamoja na kutengwa kwa vituo maalumu kuwa vimelenga kumkomboa mkulima ili aweze kunufaika na kilimo chake.

Rumuri alifafanua kuwa utaratibu wa stakabadhi gharani umewekwa kisheria hivyo hawataweza kumfumbia macho mtu yeyote atakaye kiuka utaratibu huo wa kisheria .

Aliongeza kuwa kunaumuhimu watu kuufuata ili kuisaidia serikali kupata takwimu uzalishaji wa mazao hao pamoja na kaisi kilichouzwa na kubaki na kusaidia ukusanyaji wa matapo kwa halmashuri,fedha za mapato zitakazo saidia ujenzi wa miradi mbali mbali kwenye jamii.

Kaimu Afsa Kilimo wa Wilaya ya Tanganyika Yusuph Mukhandy amewaomba wakulima wote kuwa wanazingatia utaratibu uliowekwa kwa ajili ya manufaa yao.

Vilevile kutokana na kuwa mfumo huo kuwa mara ya kwanza kutamburishwa wakulima wanapaswa kuepuka kuuza mazao yao kienyeji ambapo kwa kufanya hivyo hawataweza kunufaika na kilimo chao.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja