Skip to main content

MWENYEKITI WA KIJIJI KWA MBARONI KWA TUHUMA ZA KUOMBA RUSHWA YA LAKI MBILI.



 

  Na Mwandishi wetu

          Katavi .


TAASISI ya kuzuia na kupambana  na Rushwa(TAKUKURU)  Mkoa wa  Mkoa wa Katavi  inatarajia kuwafikisha  Mahakamani watuhumiwa watatu waliowakamatwa  wakitenda makosa ya kuomba na kupokea Rushwa  kinyume na  kifungu  cha 15(1)  (a) na (b) cha sheria  ya kupambana na Rushwa  namba   11 ya mwaka 2007 akiwemo Mwenyekiti wa Kijiji cha Vikonge Wilaya ya Tanganyika  Joseph  Sungura (53) aliyekamatwa kwa kosa la kuomba na kupokea Rushwa ya Tshs 200,000.

Mkuu wa Takukuru  Mkoa wa Katavi  Christopher  Nakua  aliwaambia wandishi wa Habari kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika maeneo tofauti ya Wilaya  za Mpanda na Tanganyika .

 Katika tukio la kwanza Takukuru  ilimkamata  Mwenyekiti wa Kijiji cha Vikonge  ambae anadaiwa  alimwita kwenye ofisi yake  mlalamikaji wa tukio hili  ambae alikuwa akifanya kazi kijijini hapo ya  kununua mazao  kwa niaba ya tajiri yake anaeishi Dar  es salaam ambae wakati wa ununuzi wa mazao hayo alikura hasara  na kushindwa kurudi kwa tajiri wake 

 Nakua alieleza kuwa ndipo Mtuhumiwa  Joseph Sungura  alipomfuata mlalamikaji  na kumweleza kuwa  anatafutwa na tajiri  yake  hivyo ili  yeye Mwenyekiti  aendelee kumlinda  anatakiwa  ampatie   kiasi cha Tshs 200,000 .

 Kwa kuonyesha  msisitizo  wa mahitaji ya fedha hizo  mtuhumiwa alimnyang'anya mlalamikaji  baiskeli  aliyokwenda nayo kwenye ofisi ya Kijiji hicho  ikiwa na pampu  ya kunyunyizia  dawa za  wadudu .

 Nakua alieleza kuwa Takukuru  walipata taarifa za mwenyekiti huyo kuomba   Rushwa na kuwa amenyang-anya  mlalamikaji baiskeli yake  waliweza kufika hadi  nyumbani kwa mtuhumiwa  na waliweza kuvikuta vitu hivyo  na alipo  ulizwa hakuwa na maelezo yoyote .

Mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa leo Mahakamani  kwa tuhuma za kushawishi  na kuomba  rushwa kinyume  na kifungu  cha 15(1)  (a) cha sheria ya kuzuia  na kupambana  na Rushwa  namba 11 ya mwaka 2007.

 Katika tukio jingine  Mkuu wa Takukuru  Mkoa wa Katavi amesema wamewakamata watu wawili  Justina  Mgamba   Mkazi wa Kijiji cha Kanoge Wilaya ya Mpanda na  Mohamed  Kajenje  Mkazi wa Kijiji cha Igalula  Wilaya ya Tanganyika  watuhumiwa hao  ni wajumbe  wa jumuia ya   Bonde  la Mto Mpanda  waliomba na kupokea Rushwa ya Tshs 50,000.


 Alisema watuhumiwa hao  mnamo machi 18 mwaka huu wakiwa   katika  operesheni  ya  kuwaondoa  na kuwaadhibu watu  waliolima  na kufanya shughuli  za kibinadamu  ndani ya eneo la mita  60 kutoka kwenye bonde la mto mpanda  walimkuta mlalamikaji akiwa amelima ndani ya mita 60 kutoka kwenye mto .


Ambapo kulingana  na sheria ya usimamizi  wa rasilimali  maji  namba 11 ya mwaka 2009  alitakiwa kulipa faini  kati ya Tshs 500,000 na 1,000,000  lakini watuhumiwa hao waliomba  na kupokea rushwa ya Tshs 50,000  ili   wasimlipishe faini kubwa  ndipo Takukuru walipopata taarifa na waliandaa mtego na kufanikiwa kuwakamata .

 Nakua alisema watuhumiwa hao  wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani  kwa kosa la  kuomba na kupokea rushwa  kinyume na kifungu  cha 15(1)   (a)     na    (b)  cha sheria ya  kuzuia na  kupambana na rushwa  namba 11 ya  mwaka 2007.

Takukuru  Mkoa wa Katavi  wanatowa wito  kwa watumishi  wa umma na jamii kutojihusisha  na vitendo vya   kijinai  kama kuomba na kupokea rushwa  kwa  sababu  zozote  zile .
   

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...