Skip to main content

MWENYEKITI WA KIJIJI KWA MBARONI KWA TUHUMA ZA KUOMBA RUSHWA YA LAKI MBILI.



 

  Na Mwandishi wetu

          Katavi .


TAASISI ya kuzuia na kupambana  na Rushwa(TAKUKURU)  Mkoa wa  Mkoa wa Katavi  inatarajia kuwafikisha  Mahakamani watuhumiwa watatu waliowakamatwa  wakitenda makosa ya kuomba na kupokea Rushwa  kinyume na  kifungu  cha 15(1)  (a) na (b) cha sheria  ya kupambana na Rushwa  namba   11 ya mwaka 2007 akiwemo Mwenyekiti wa Kijiji cha Vikonge Wilaya ya Tanganyika  Joseph  Sungura (53) aliyekamatwa kwa kosa la kuomba na kupokea Rushwa ya Tshs 200,000.

Mkuu wa Takukuru  Mkoa wa Katavi  Christopher  Nakua  aliwaambia wandishi wa Habari kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika maeneo tofauti ya Wilaya  za Mpanda na Tanganyika .

 Katika tukio la kwanza Takukuru  ilimkamata  Mwenyekiti wa Kijiji cha Vikonge  ambae anadaiwa  alimwita kwenye ofisi yake  mlalamikaji wa tukio hili  ambae alikuwa akifanya kazi kijijini hapo ya  kununua mazao  kwa niaba ya tajiri yake anaeishi Dar  es salaam ambae wakati wa ununuzi wa mazao hayo alikura hasara  na kushindwa kurudi kwa tajiri wake 

 Nakua alieleza kuwa ndipo Mtuhumiwa  Joseph Sungura  alipomfuata mlalamikaji  na kumweleza kuwa  anatafutwa na tajiri  yake  hivyo ili  yeye Mwenyekiti  aendelee kumlinda  anatakiwa  ampatie   kiasi cha Tshs 200,000 .

 Kwa kuonyesha  msisitizo  wa mahitaji ya fedha hizo  mtuhumiwa alimnyang'anya mlalamikaji  baiskeli  aliyokwenda nayo kwenye ofisi ya Kijiji hicho  ikiwa na pampu  ya kunyunyizia  dawa za  wadudu .

 Nakua alieleza kuwa Takukuru  walipata taarifa za mwenyekiti huyo kuomba   Rushwa na kuwa amenyang-anya  mlalamikaji baiskeli yake  waliweza kufika hadi  nyumbani kwa mtuhumiwa  na waliweza kuvikuta vitu hivyo  na alipo  ulizwa hakuwa na maelezo yoyote .

Mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa leo Mahakamani  kwa tuhuma za kushawishi  na kuomba  rushwa kinyume  na kifungu  cha 15(1)  (a) cha sheria ya kuzuia  na kupambana  na Rushwa  namba 11 ya mwaka 2007.

 Katika tukio jingine  Mkuu wa Takukuru  Mkoa wa Katavi amesema wamewakamata watu wawili  Justina  Mgamba   Mkazi wa Kijiji cha Kanoge Wilaya ya Mpanda na  Mohamed  Kajenje  Mkazi wa Kijiji cha Igalula  Wilaya ya Tanganyika  watuhumiwa hao  ni wajumbe  wa jumuia ya   Bonde  la Mto Mpanda  waliomba na kupokea Rushwa ya Tshs 50,000.


 Alisema watuhumiwa hao  mnamo machi 18 mwaka huu wakiwa   katika  operesheni  ya  kuwaondoa  na kuwaadhibu watu  waliolima  na kufanya shughuli  za kibinadamu  ndani ya eneo la mita  60 kutoka kwenye bonde la mto mpanda  walimkuta mlalamikaji akiwa amelima ndani ya mita 60 kutoka kwenye mto .


Ambapo kulingana  na sheria ya usimamizi  wa rasilimali  maji  namba 11 ya mwaka 2009  alitakiwa kulipa faini  kati ya Tshs 500,000 na 1,000,000  lakini watuhumiwa hao waliomba  na kupokea rushwa ya Tshs 50,000  ili   wasimlipishe faini kubwa  ndipo Takukuru walipopata taarifa na waliandaa mtego na kufanikiwa kuwakamata .

 Nakua alisema watuhumiwa hao  wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani  kwa kosa la  kuomba na kupokea rushwa  kinyume na kifungu  cha 15(1)   (a)     na    (b)  cha sheria ya  kuzuia na  kupambana na rushwa  namba 11 ya  mwaka 2007.

Takukuru  Mkoa wa Katavi  wanatowa wito  kwa watumishi  wa umma na jamii kutojihusisha  na vitendo vya   kijinai  kama kuomba na kupokea rushwa  kwa  sababu  zozote  zile .
   

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja