Skip to main content

MGANGA MKUU WA MKOA WA KATAVI ATAKIWA KUJIELEZA KWA KUKIUKA AGIZO LA RC HOMERA DHIDI YA CORONA.



Ni baada ya wahamiaji haramu watano waliokamatwa na maafisa wa uhamiaji kushindwa kufanyiwa vipimo.


Na Mwandishi Wetu,
      Katavi.

MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Omary Sukari anapaswa  kujieleze kutokana na kukiuka maagizo aliyopewa March 28 mwaka huu kwenye kikao cha dharura PHC cha maelekezo ya kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya Corona.,

Kikao hicho ambacho kililenga pia kusambaza muongozo wa karatini kwa wageni wote wanaoingia mkoani humo kupitia njia mbali mbali za usafiri kama vile wa mabasi na meli ambapo yalitolewa maadhimio ya kuhakikisha kila eneo la mpaka wa Mkoa linakuwa na kituo  maalumu cha kizuizi kwa ajili ya ukaguzi wa kitabibu na karatini pamoja na wataalamu wa afya ili kabla ya mtu hajaingia mjini apimwe kwanza.

Akitoa kauli hiyo Mkuu wa Mkoa wa Katavi Comrade Juma Homera baada ya kufanya 
ukaguzi wa kushitukiza ili kuona utekelezaji wa maagizo yake katika kituo cha kizuizi cha Milala ambapo hakukuta muuguzi yeyote wa afya mahali pale

Homera amesema wengine wanaotakiwa kujieleza ni Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpanda na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika ambao kwa pamoja wameonekana kushindwa kutekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa huyo.

Licha ya kutoa maagizo hayo kwa maafisa hao kujieleza haraka iwezekanavyo ameitaka idara ya afya ihakikishe inaweka vizuizi huku wakiwepo na wauguzi ambao watakuwa na kazi maalumu ya kupima watu wote wanaoingia mkoani humo na wale watakao bainika kuwa na vurusi vya corona wawezi kuwekwa kwenye karatini.

Vilevile amevitaka vyombo vya usalama mkoani Katavi kuhakikisha vinafanya ukaguzi wa kutosha ili kutambua raia wanaoingia wanatambulika.

Katika idara ambayo imefanikiwa kutekeleza maagizo ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ni Idara ya uhamiaji pekee.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera



Kamishina Msaidizi wa uhamiaji Mkoa wa Katavi Vicent Haule amesema baada ya kupata maagizo 
 hayo ya Mkuu wa Mkoa mara moja walitekeleza maagizo kwa sababu wanatambua umuhimu wa suala hilo ili kuweza kukabiliana na kuenea kwa kwa virusi vya corona

Vicent amebainisha kuwa wamefanikiwa kukamata wahamiaji haramu watano ambao walitaka  kuvuka kinyume cha utaratubu wa sheria za nchi  huku juhudi za kupimwa ziligonga mwamba kwa kuwa kwenye kituo hicho cha Milala hapakuwa na muuguzi hata mmoja wa afya.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Omary Sukari



Nao baadhi ya wananchi kwa wakati tofauti Paulina Mwasha,Anthony na Wande Juma wamesema kuwa kitendo cha kukosekana kwa wahudumu wa afya katika vizuizi ni hatari sana kwa mkoa wa Katavi kwani kunauwezekano watu wenye maabukizi ya virusi vya corona wakaingia.

Hivyo wamemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera kwa kuchukua hatua sitahiki za kumtaka mganga mkuu wa Mkoa kutoa maelezo ya kutosha kuwa kwanini ameruhusu uzembe kama huo ujitokeze huku akifahamu kuwa dunia iko kwenye mapambano dhidi ya corona.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...