Skip to main content

Posts

Utacheka//Maneno ya Kingereza yalivyowashinda kwa Kiswahili.

Wahudumu wa kujitolea Ruvuma wapewa msaada wa Baiskeli 15.

Miongoni mwa wahudumu wa kujitolea mkoani Ruvuma waliopewa msaada wa baiskeli 15 kutoka kutoka shirika la SATFkupitia ubalozi wa Marekani. Katikati ni Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema akikata utepe kuzindua baskeli 15 zilizotolewa na ubalozi wa Marekani kwa wahudumu wa kujitolea Mkoa wa Ruvuma. Na Albano Midelo Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma Wahudumu 15 wa kujitolea ngazi ya Jamii ambao wamekuwa wanafanyakazi ya kuwasaidia watoto wa kaya masikini 423 mkoani Ruvuma wamepewa msaada wa baiskeli ili kuwasaidia kutoa huduma kwa jamii. Msaada huo umetolewa na Shirika la Social Action Trust Fund(SATF) kwa udhamini wa mfuko wa dharura wa Rais wa Marekani wa kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI(PEPFAR), kupitia mfuko wa Balozi wa Marekani nchini Tanzania. Akitoa taarifa kwa Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Pololet Mgema katika hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Songea ,Mwakilishi wa Mkurugenzi wa SATF...

Wazee wa Mkoa wa Ruvuma waunda Baraza la Wazee.

Wawakilishi wa wazee wa Mkoa wa Ruvuma kutoka wilaya  zote tano wakiwa katika kikao maalum cha kuunda Baraza la wazee wa Mkoa pamoja na kuchagua viongozi watakaoongoza Baraza hilo ngazi ya Mkoa wa Ruvuma. Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali watu akifungua kikao maalum cha uundaji wa Baraza la wazee Mkoa wa Ruvuma na kufanya  uchaguzi wa kuwapata viongozi watakaoliongoza baraza hilo ngazi ya Mkoa. Na Albano Midelo Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma Wazee wa Mkoa wa Ruvuma wamefanya kikao maalum cha uundaji Baraza la Wazee la Mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa mipango Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea. Waliochaguliwa kuunda Baraza hilo kwenye uchaguzi ulishirikisha wawakilishi kutoka wilaya za Nyasa,Mbinga,Songea,Tunduru na Namtumbo ni pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa amechaguliwa Elenzian Nyoni kutoka Manispaa ya Songea. Wengine waliochaguliwa ni Lusiana Nduguru kutoka Halmashauri ya Mji wa Mbin...

Furahi na Watoto wakicheza Ngoma ya asili, Staili yao utaipenda

Sababu Vifo vitokanavyo na Uzazi na Vifo vya Watoto//Watoto 613 walipote...

Wakulima wa Pamba wawaondolea uvivu Wanunuzi mbele ya RC//Bei yawakonga ...

Viwanja 8725 vimepimwa kipindi cha 2020/21 ukilinganisha na Viwanja Elfu...