Na Swaum Katambo-Katavi Sheria mpya ya Madini ya uongezaji thamani madini chini ya kifungu cha 129 iloyopitishwa Agosti 28, 2020 inayoruhusu kusafirisha Makinikia nje ya Nchi yenye kiwango cha shaba kisichopungua asilimia 20 imesaidia kusafirisha Tani 508.9 z a makinikia kutoka mgodi wa Katavi Mining Co.Ltd kwenda nje ya Nchi kwa mara ya kwanza . Meneja wa Mgodi wa Katavi Mining Company Ltd Ndg Twalib Mohamed Seif ameyasema hayo leo tarehe 2 Machi 2021 wakati akitoa taarifa ya mgodi huo mbele ya Waziri Wa Nchi Ofisi Rais Uwekezaji Prof. Kitila Alexandra Mkumbo alipotembelea Kiwanda ni h apo na kubainisha kuwa jumla ya malipo yanayotokana na usafirishaji wa kwanza wa Makinikia ya Shaba ni kiasi cha Shilingi za kitanzania 449,251,452.22 Hata hivyo Twalib ameiomba Serikali i wapatie umeme wa uhakika ili kupunguza gharama za uzalishaji kwani kwa sasa wanatumia J enereta kwa shughuli za uwezeshaji Mgodi . Pia ameiomba Serikali kusaidia kutengeneza baraba...