Skip to main content

SHERIA MPYA YA MADINI YAPELEKEA TANI 508.9 KUSAFIRISHWA NJE YA NCHI

Na Swaum Katambo-Katavi

Sheria mpya ya Madini ya uongezaji thamani madini chini ya kifungu cha 129 iloyopitishwa Agosti 28, 2020 inayoruhusu kusafirisha Makinikia nje ya Nchi yenye kiwango cha shaba kisichopungua asilimia 20 imesaidia kusafirisha Tani 508.9 za makinikia kutoka mgodi wa Katavi Mining Co.Ltd kwenda nje ya Nchi kwa mara ya kwanza.

Meneja wa Mgodi wa Katavi Mining Company Ltd Ndg Twalib Mohamed Seif ameyasema hayo leo tarehe 2 Machi 2021 wakati akitoa taarifa ya mgodi huo mbele ya Waziri Wa Nchi Ofisi Rais Uwekezaji Prof. Kitila Alexandra Mkumbo alipotembelea Kiwandani hapo na kubainisha kuwa jumla ya malipo yanayotokana na usafirishaji wa kwanza wa Makinikia ya Shaba ni kiasi cha Shilingi za kitanzania 449,251,452.22

Hata hivyo Twalib ameiomba Serikali iwapatie umeme wa uhakika ili kupunguza gharama za uzalishaji kwani kwa sasa wanatumia Jenereta kwa shughuli za uwezeshaji Mgodi.

Pia ameiomba Serikali kusaidia kutengeneza barabara yenye urefu wa Km 8 kutoka barabara kuu iendayo Sumbawanga hadi eneo la mgodi.

Kadhalika Seif ameiomba Serikali kupitia Ofisi ya Madini Mpanda mkoani Katavi kuwapatia Mwongozo na usimamizi ili kuweza kufanikisha ununuzi wa Malighafi kutoka kwa wachimbaji wadogo.

Kuhusu barabara, Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera  amesema kuwa ili kutatua Changamoto hiyo serikali inaendelea kulifanyia kazi ambapo kwa ushirikiano na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) itatengenza.

Pia ameupongeza uongozi wa Katavi Mining Company Ltd kwani uwekezaji wao unaingizia Halmashauri kipato.

Kwa upande wake Waziri Wa Nchi Ofisi Rais Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo ameupongeza uongozi wa Katavi Mining Company Ltd kwa kufanya kazi nzuri huku akiitambua changamoto kubwa ya upatikanaji wa Umeme unaozikabili Kampuni za uwekezaji Mkoani Katavi hadi kupelekea kushindwa kufanya vizuri shughuli za uwekezaji.

Akizungumza na Mwekezaji wa Mgodi wa Katavi Mining Company Ltd Eng. Mahmoud Abdulrazack, Waziri Mkumbo amepongeza Sheria ya Madini ya Mwaka 2017 na Kanuni zake na kusema kuwa baada ya Sheria hiyo wawekezaji wengi wa sekta ya Madini kutoka nchini Oman wamependezwa na uwekezaji nchini Tanzania.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...