Skip to main content

MKUU WA MKOA WA RUVUMA AAGIZA VYANZO VYA MAJI SONGEA KULINDWA.


 
    

                 ********************************
                                   Na,Mwandishi Wetu-Songea.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amekagua vyanzo vya maji kwenye miradi ya maji Ndongosi na Liula wilayani Songea na kuagiza vyanzo hivyo kulindwa ili viwe endelevu.

Brigedia Jenerali Ibuge amesikitishwa na uharibifu wa vyanzo hivyo unaoendelea kufanywa na wananchi kwa kulima mazao na shughuli nyingine za kibinadamu hali inayosababisha vyanzo hivyo kuwa katika hatari ya kutoweka.

“Naagiza kila kijiji kuitisha mkutano mkuu wa kijiji,kati ya ajenda zake kuu,iwe ni namna gani ya kukabiliana na tabia hii ya kuharibu vyanzo vya maji,nimeona miti inavyoangushwa kama haina mwenyewe’’,alisema RC Ibuge.

Hata hivyo alisema serikali inapenda watu wajipatie kipato kutokana na kilimo,ametahadharisha kuwa shughuli za kinadamu ndizo zinazoathiri vyanzo vya maji.

Ametoa rai kwa watalaam wote wa maji wakiwemo RUWASA na Bonde la Maji la Ziwa Nyasa,waende vijijini ili kutoa elimu ya mazingira kwa wananchi na kuweka ramani kwenye eneo zima ambalo lenye vyanzo vya maji ambapo ameagiza utekelezaji wa maagizo hayo ufanyike kabla ya Desemba Mosi mwaka huu.

“Tusiseme tuna changamoto ya tabianchi ni sisi wenyewe ndiyo tunaoharibu kwa kukamata miti,kulima hadi kwenye kingo za mito ,tunachoma moto misitu na kuvunja sheria mbalimbali za mazingira’’,alisema RC Ibuge.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji ya kijiji cha Ndongosi na Liula kwa Mkuu wa Mkoa,Meneja RUWASA Wilaya ya Songea Mhandisi Mathias Charles alisema mradi wa maji Ndongosi ulisanifiwa kwa zaidi ya shilingi milioni 332.

Hata hivyo alisema kati ya fedha hizo zaidi ya shilingi milioni 23 ni fedha za maandalizi ya mradi,zaidi ya shilingi milioni 51 ni za usimamizi na zaidi ya shilingi milioni 256 ni fedha za ujenzi wa mradi wa maji.

Ameutaja mradi wa maji Ndongosi ulisanifiwa kuhudumia wakazi wapatao 3,175 wenye mahitaji ya maji lita 119,062.5 kwa siku na kwamba chanzo cha maji kutoka mto Mlaimonga kina uwezo wa kuzalisha maji lita 902,016 kwa siku na kwamba mradi umefikia asilimia 98.

Kuhusu mradi wa maji wa kijiji cha Liula,Mhandisi huyo wa maji amesema mradi huo awali, ulisanifiwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni moja ambapo RUWASA kwa kutumia watalaam wake wa ndani wamefanikiwa kumaliza shughuli zote kwa shilingi milioni 56 ambapo mradi umekamilika na unahudumia watu wapatao 4,320.

Hata hivyo amezitaja changamoto kuu zinazoikabili miradi hiyo ni uharibifu wa vyanzo vya maji unaofanywa na wananchi kwa kuchoma moto hovyo,kulima kwenye vyanzo na kukata miti.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 30,2021

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...