Skip to main content

Wilaya ya Nyasa yatoa mikopo kwa Asilimia 100,RC Ibuge apongeza.


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akizungumza katika mkutano maalum wa CAG Halmashauri ya wilaya ya Nyasa katika ukumbi wa Kapteni Komba mjini Mbambabay.


Na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali  Wilbert Ibuge,ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwa kutoa mikopo kwa asilimia 100  yenye thamani ya ya zaidi ya shilingi milioni 66.6 kwa  makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

RC Ibuge ametoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki katika mkutano maalum wa Baraza la madiwani la Halmashauri hiyo wa kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG kwa mwaka 2019/2020.

Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Kepteni John Komba mjini Mbambabay Makao makuu ya Wilaya ya Nyasa.

Brigedia Jenerali Ibuge amepongeza mara ya kwanza Halmashauri hiyo kutoa mikopo kwa asilimia 100 ambapo kati ya fedha zilizotolewa Wanawake wamepata milioni 37.6 vijana, milioni 19,000,000 kundi la watu wenye ulemavu shilingi milioni 10,000,000.

Katika hatua nyingine RC Ibuge ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kufanikiwa kukusanya mapato ya ndani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.2 ambayo ni sawa na  asilimia 82.95.

“Kwa moyo wa dhati kabisa naipongeza Halmashauri hii kwa kutoa mikopo kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa kuwa makundi hayo ni muhimu katika Uzalishaji mali”,alisisitiza RC Ibuge.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amewaagiza Madiwani na watendaji wa Halmashauri kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuweza kuinua makusanyo na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa asilimia 100.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mhe.Stewart Nombo ameahidi kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa kwa maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...