Skip to main content

UJENZI NA UKARABATI MIUNDOMBINU YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI WAANZA MADIBILA.

Kulia Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali Akimkabidhi Mkataba wa Ujenzi wa Miundombinu katika Skimu ya Kilimo cha Umwagiliaji Madibila Bw. David Noble Mkurugenzi wa Kampuni ya Ukandarasi ya White City International.


Bw.Shabani Sawasawa (mkulima) akizungumzia manufaa ya Mradi wa Regrow katika skimu ya kilimo cha Umwagiliaji ya Madibila, iliyopo katika Halmashauri ya Mbarali.

Na. Mwandishi Wetu –Mbarali,Mbeya.

Ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kilimo cha Umwagiliaji katika skimu ya Madibila iliyopo katika Halmashauri ya Mbarali Mkoani Mbeya, umeanza Rasmi kwa mkandarasi kukabidhiwa eneo la ujenzi wa mradi na mkataba kwa utekelezaji wa mradi huo, ambao una lengo la kusimamia ustahimilivu wa maliasili kwa ajili ya ukuaji wa utalii na shughuli mbadala za kiuchumi kusini mwa Tanzania.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Daudi Kaale, amesema Tume hiyo ina jukumu kubwa ya kusimamia kilimo cha umwagiliaji nchini na kuhakikisha kwamba Skimu ya kilimo kama ya Madibila inafikia malengo yaliyokusudiwa. 

“Uzoefu unaonesha kuwa serikali imejenga skimu nyingi kwa gharama kubwa lakini baada ya muda hazitekelezi kazi zake au majukumu kama ilivyokusudiwa, tija na uzalishaji kupungua na hata mundombinu kuharibika.” Alisema Kaale.

Alisisistiza kuwa kuanzia sasa ni hazma ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kuhakikisha kuwa miundombinu yote inarejea katika hali yake ya kawaida na kufanya kazi katika malengo yaliyokusudiwa, ili kuongeza pato la Taifa, kuondoa umaskini na kuhakikisha ongezeko la ajira kwa wananchi.

Akiongea katika makababidhiano hayo msimamizi wa Mradi huo kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mhandisi Mkuu Ebenezer Kombe amesema, yeye kama Msimamizi Mkuu, ana jukumu la kusimamia ubora, gharama halisi za ujenzi na muda wa miezi 18 ambao umepangwa kwa kazi kukamilika.

Kwa upande wake Muwakilishi wa Mkandarasi kampuni ya wazawa White City Internatinal, Bwana. David Noble amesema, wakulima watapata nafasi ya kuendelea na shughuli zao za kilimo wakati ujenzi ukiendelea, na watajitahdi kufanya kazi kwa kiwango na wakati.

Bw. Shabani Juma Sawasawa ni mkulima katika eneo hilo, amesema kuwa, ujio wa mradi utakuwa na manufaa ya kuokoa upotevu wa maji baada ya ujenzi wa mfereji wenye urefu wa kilikometa tatu kukamilika “Wakulima tutanufaika na kutunza maji pamoja na kuyaruhusu yaende katika mto Ruaha Mkuu kwa matumizi ya viumbe hai wengine, Maliasili na Mazingira.”Alisisitiza

Mradi huo wa REGROW ni Mradi wa usimamizi stahimilivu wa maliasili kwa ajili ya ukuaji wa utalii na shughuli mbadala za kiuchumi kusini mwa Tanzania, Mradi ambao unafadhiliwa na Benki ya Dunia kwa kushirikiana na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...