Skip to main content

ALIYEKUWA DC MLELE AMUOMBA DC MPYA KUSIMAMIA NA KUMALIZIA MIRADI INAYOENDELEA.


 
Na. Swaum Katambo

Katika makabidhiano ya Ofisi,aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda amemuomba Mkuu mpya wa Wilaya hiyo Filberto Sanga kusimamia vifaa vinavyotakiwa kuletwa kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa Hospitali za Wilaya zilizopo Mlele na Mpimbwe ili ziweze kufanya kazi vizuri pindi zitakapomalizika.

Kasanda amemuomba DC Sanga pia kusimamia kwa ukaribu ukamilishaji wa Ujenzi wa Kituo cha Afya Ilunde kilichopo Kata ya Ilunde Halmashari ya Wilaya ya Mlele kwakuwa kipo mbali na mjini hivyo kupelekea vifaa vya Ujenzi kutofika kwa kutosha na kwa wakati.

"Watu wa Ilunde wapo mbali na sisi,mvua ikianza kunyesha wanawake wajawazito wanapata Changamoto kidogo ya mawasiliano kufika kwa wakati,nikuombe tuu kifuatilie kile kituo kwa ukaribu,ukifanyie kazi mpaka masika yanaanza wale kinamama na watu waliopo kwenye ile Kata waweze kupata huduma ya kutosha"Alisema Kasanda

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda akimuomba Mkuu mpya wa Wilaya hiyo Filberto Sanga kusimamia utekelezaji wa Miradi inayoendelea

Kadhalika,amemuomba DC Sanga kufuatilia kwa ukaribu ukamilishaji wa Miradi mbalimbali inayoendelea kujengwa ikiwemo Miradi ya Nyumba za Wakuu wa Idara Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe,Ofisi za Wakurugenzi,Miradi ya Elimu ikiwemo na Madawati na kusema kuwa yupo tayari kumpa ushirikiano endapo kuna mahali kutamtatiza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filberto Sanga mara baada ya kukabidhiwa Ofisi ameahidi kuyafanyia kazi yote aliyoshauriwa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Rachel Kasanda na kuiomba timu yote iliyofanya kazi na mtangulizi wake kuendelea kumpa ushirikiano.


Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mhe.Filberto Sanga

Nae Lucas Kifyasi Mwakilishi wa  Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kwa niaba ya Wakurugenzi wote (Mlele na Mpimbwe) amemshukuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Rachel Kasanda kwa ushirikiano alioutoa kwao huku wakiahidi kutoa ushirikiano kwa DC Sanga kwa kufanya vizuri kiutendaji na katika ukusanyaji wa Mapato ya ndani.


Lucas Kifyasi Mwakilishi wa  Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja