Skip to main content

RUWASA Songea yatoa mafunzo na vyeti kwa jumuiya tisa za watumia maji




Katibu Tawala Wilaya ya Songea Pendo Ndumbaro akigawa vyeti kwa wanajumuiya za maji wilaya ya Songea baaada ya kupata mafunzo kutoka RUWASA wa maji vijijini 

RUWASA wilaya ya Songea mkoani Ruvuma imetoa mafunzo na kugawa vyeti kwa jumuiya tisa za watuamia maji katika Halmashauri za Madaba na Halmashauri ya Songea.

Akizungumza katika mafunzo hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Songea Klub Mtaalam wa RUWASA Wilaya ya Songea Samweli Sanya amesema Ruwasa kwa kushirikiana na jumuiya hizo zilizoundwa watahakikisha wananchi wanapata huduma ya maji endelevu kwa usimamizi na uendeshaji na wananchi watachangia huduma hiyo.

Mgeni rasimi katika mafunzo hayo Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea Pendo Ndumbaro amesema lengo la RUWASA ni kutekeleza na kuiwezesha jamii kuwa na jumuiya ya maji imara na kuleta tija endelevu kwa wananchi vijijini.

Amesema Jumuiya waliopata mafunzo hayo wawe walimu na wasimamizi wazuri katika kutunza miundo mbinu iliyopo katika jumuiya za watumia maji ili wananchi wapate huduma bora na endelevu.

‘’Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuunda wakala wa maji safi na mazingira vijijini RUWASA inatusaidia kuleta huduma nzuri karibu na wananchi wa vijijini’’,alisema.



Jumuiya tisa za maji  katika wilaya ya Songea zikipewa mafunzo ya watumia maji kutoka  RUWASA yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Songea klub

Ndumbaro amesisistiza kuwa Jumuiya tisa zilizopata mafunzo hao zihakikishe wananchi wanapata huduma nzuri ya maji na watunze mazingira,Serikali imetoa fedha nyingi katika miradi mikubwa ya maji ambapo amewaasa wananchi kutunza vyanzo vya maji na kuacha kukata miti hovyo.

‘’Nitolee mfano mzuri katika milima ya Lihanji wilayani Songea kuna vyanzo vya maji na vyanzo vyake vinalisha maeneo makubwa katika tarafa ya Ruvuma Peramiho na Kilagano vinatumia kutoka milima ya Lihanji’’,alisisitiza.

Amesema licha ya mafunzo waliyopata kuna rasimu ambazo zimetolewa na kupitishwa Jumuiya zote ambazo ameagiza wakasimamie na kwamba miundombinu inapoharibika irekebishwe kwa kutumia michango wanayochangisha kwa wananchi.

RUWASA imeanzisha kupitia sheria namba tano iliyopitishwa na Bunge mwaka 2019 na kuanza kutumika Julai mosi 2019.

Imeandikwa na Anet Ndonde
Ofisi ya Habari Mkoa wa Ruvuma

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...