![]() |
| Mkuu wa Mkoa wa Katavi Comrade Juma Homera wa kwanza kutoka kulia akikabidhiwa box ya vifaa kutoka shirika la WalterReed na Dkt Shabain Ndama wa kwanza kutoka kushoto kwenye picha. |
Na Mwandishi Wetu
Katavi
Serikali ya
Mkoa wa Katavi katika kuendelea kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19 imefanikiwa kupokea vifaa tiba kutoka shirika la WalteReed vyenye thamani
ya milioni ishirini na tano ili kuhakikisha mkoa huo haupatikani na mgonjwa
hata mmoja wa virusi hivyo.
Mkoa huo
hapo awali ulikabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa vitendea kazi kama vile
Scaner kwenye baadhi ya vituo vya
vizuizi kwenye mipaka yake ya Burudi na
DRC Congo.
Akikabidhi
vifaa hivyo Meneja Mradi WalterReed (HJFMRI) Mkoa wa Katavi Dkt Shabain Ndama mbele ya Mkuu wa Mkoa huo Juma Homera amesema kuwa vifaa hivyo vimetolewa ili
kuendelea kuthibiti maambukizi ya
ugonjwa wa COVID 19.
Ndama alieleza
kuwa vifaa hivyo vimetolewa kwa awamu ya kwanza
ni Scaner sita vya kisasa kwa ajili ya kupima joto la mwili,Madawa za
kuuwa wadudu picks 300,Grovs pea 72 pamoja na Dawa za kuuliza maumivu ambavyo
vimegharimu jumla ya milioni ishirini na tano.
Pia wanatarajia kuleta katika awamu ya pili ni vitakasa mikono na barakaoa ambavyo
vitasaidia watu kutumia ili kujikinga na maabukizi ya COVID 19.
Juma Homera
Mkuu wa Mkoa wa Katavi akizungumza baada ya kupokea vifaa hivyo mbali na kuwa
pongeza walterReed amewata walaamu wa afya kuhakikisha vifaa vinafika sehemu
husika ili kukabiriana na Corona.
Mkuu wa mkoa
huo ametoa wito kwa Madaktari kuendelea kutumia vifaa hivyo kwa uagalifu kwa
sababu vifaa vilivyopobado ni vichache na kwa namna ambavyo wanaendelea kupokea
vifaa kutoka kwa wadau mbalimbali vitasaidia mapambano hayo.
“katika
maeneo ya mipaka hususani Mishamo wilaya ya Tanganyika hatukuwa na vifaa ambapo
kuna wageni wengi kutoka nchi ya Burudi
wanao zunguka hadi Mkoa wa Kigoma na wengine wanaigilia ziwa Tanganyika
kutoka nchi ya DRC Congo …pamoja na eneo la kata ya Kasakatengule huko kote
hatukuwa na Scaner” Alisema Homera.
Pamoja na
hayo Mkuu wa Mkoa huyo alisema kuwa hadi sasa katika mkoa wamefanikiwa kuweka
watu wanne Karatini huku kukishuhudiwa kuwa hakuna mtu hata mmoja
aliyepatikana na maabukizi ya COVID 19.
Magaga Mkuu
wa Mkoa wa Katavi Dkt Omary Sukari aliweka wazi kuwa kabla ya kupata vifaa
hivyo kupatikana walikuwa wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa vifaa.
Hivyo Dkt
Sukari alisema kuwa vifaa hivyo vitasaidia sana katika mapambono ya COVID 19 na
kuwajengea uhakika wa kazi wanayoifanya kama madaktari ya kutokomeza virusi
hivyo.

Comments
Post a Comment