Skip to main content

MAMANTILIE WACHANGIA FEDHA MAPAMBANO YA CORONA ,WAZIRI MKUU AKOLEZA VITA YA COVID-19






Na Mwandishi wetu
      Dar es salaam.


WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewaomba watu wote nchini kuendelea kukabiliana na ugonjwa wa corona ili kuzuia kusambaa zaidi.

Hayo ameyasema waziri mkuu huyo baada ya kukabidhiwa vifaa kinga,fedha na dawa kutoka taasisi,Mampuni na Umoja wa Mamantilie .

Kassim Majaliwa amesema kuwa watanzania wanapaswa kuzingatia kuchukua tahadhari kama vile kunawa mikono mara kwa mara kwa maji safi na salama yanayotiririka pamoja na kuepuka misongamano ili kudhibiti janga lililoikumba dunia.

"Wakati tunaendelea kukabiliana na janga hili la corona tunapaswa kujua kwamba ugonjwa huu utaleta athari za kiuchumi " amesema Majaliwa.





Hivyo pia amewashukuru watanzania waliojitokeza kuchangia fedha,dawa na vifaa kinga kwa kuwa msaada huo utakuwa na tija kwa watu wote waliokumbwa na COVID-19 pamoja na kusaidia watu wote kujikinga ili kuzuia kusambaa kwa homa kali ya mapafu.

Amesema Waziri Mkuu "Vitu vyote hivi tulivyo vipokea vinagharama kubwa,tumeona watanzania wenye moyo wamekuja hapa kuugana na serikali kukabilia na ugonjwa huu,Hivyo hatuwezi kuacha hivi bila kutoa shukrani kwa wenzetu walio toa msaada huu".

Amefafanua kuwa watanzania wanaopenda kuchangia jitihada za kukabiliana na ugonjwa huu wachangie fedha Benki Kuu kupitia Account NATIONAL RELIF FUND ELECTRONIC,Namba 9921159801 na kwamba wanaweza kuchangia kupitia Ofsi ya Waziri Mkuu na Ofsi ya Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto.



Baadhi ya Kampuni zilizochangia serikali katika kukabiliana na corona ni NMB mil 100,CRDB mil 150,Benk ya UBA mil 230,Umoja wa Mamantilie Mil 2 ,ASHTON MEDIA mil 104 na kampuni mbalimbali zimechangia fedha nna vifaa.

Wakati huo huo waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsi wazee na watoto Ummy Mwalimu amesema kuwa kwa kipindi cha masaa 24 tangu March 27 Mwaka huu jumla ya sampuli 26 zimewasilishwa maabala ya Taifa ya Afya ya jamii na zote zimethibitishwa hazina maambuki(hasi) Hivyo watu walio thibitika chanya kuwa na ugojwa huo bado ni 13.  





Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja