Skip to main content

MAMANTILIE WACHANGIA FEDHA MAPAMBANO YA CORONA ,WAZIRI MKUU AKOLEZA VITA YA COVID-19






Na Mwandishi wetu
      Dar es salaam.


WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewaomba watu wote nchini kuendelea kukabiliana na ugonjwa wa corona ili kuzuia kusambaa zaidi.

Hayo ameyasema waziri mkuu huyo baada ya kukabidhiwa vifaa kinga,fedha na dawa kutoka taasisi,Mampuni na Umoja wa Mamantilie .

Kassim Majaliwa amesema kuwa watanzania wanapaswa kuzingatia kuchukua tahadhari kama vile kunawa mikono mara kwa mara kwa maji safi na salama yanayotiririka pamoja na kuepuka misongamano ili kudhibiti janga lililoikumba dunia.

"Wakati tunaendelea kukabiliana na janga hili la corona tunapaswa kujua kwamba ugonjwa huu utaleta athari za kiuchumi " amesema Majaliwa.





Hivyo pia amewashukuru watanzania waliojitokeza kuchangia fedha,dawa na vifaa kinga kwa kuwa msaada huo utakuwa na tija kwa watu wote waliokumbwa na COVID-19 pamoja na kusaidia watu wote kujikinga ili kuzuia kusambaa kwa homa kali ya mapafu.

Amesema Waziri Mkuu "Vitu vyote hivi tulivyo vipokea vinagharama kubwa,tumeona watanzania wenye moyo wamekuja hapa kuugana na serikali kukabilia na ugonjwa huu,Hivyo hatuwezi kuacha hivi bila kutoa shukrani kwa wenzetu walio toa msaada huu".

Amefafanua kuwa watanzania wanaopenda kuchangia jitihada za kukabiliana na ugonjwa huu wachangie fedha Benki Kuu kupitia Account NATIONAL RELIF FUND ELECTRONIC,Namba 9921159801 na kwamba wanaweza kuchangia kupitia Ofsi ya Waziri Mkuu na Ofsi ya Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto.



Baadhi ya Kampuni zilizochangia serikali katika kukabiliana na corona ni NMB mil 100,CRDB mil 150,Benk ya UBA mil 230,Umoja wa Mamantilie Mil 2 ,ASHTON MEDIA mil 104 na kampuni mbalimbali zimechangia fedha nna vifaa.

Wakati huo huo waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsi wazee na watoto Ummy Mwalimu amesema kuwa kwa kipindi cha masaa 24 tangu March 27 Mwaka huu jumla ya sampuli 26 zimewasilishwa maabala ya Taifa ya Afya ya jamii na zote zimethibitishwa hazina maambuki(hasi) Hivyo watu walio thibitika chanya kuwa na ugojwa huo bado ni 13.  





Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...