Na Mwandishi Wetu. Katavi. MTU mmoja Mkazi wa Mtaa wa Mpanda Hotel katika Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi aliyejulikana kwa jina la Paulo Chundu amekufa hapo hapo baada ya kupigwa na radi akiwa anaaendesha pikipiki wakati akitokea kwenye shamba la mpunga . Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Benjamin Kuzaga aliwaambia wandishi wa habari kuwa tukio la kifo cha marehemu huyo lilitokea hapo juzi majira ya saa 12 jioni katika eneo la Kalilankuluku Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Tanganyika . Kuzaga alieleza kuwa kabla ya tukio hilo marehemu huyo alikuwa ameaga nyumbani kwake kuwa anapeleka chakula kwenye shamba lake la mpunga kwa ajiri ya chakula cha vibarua waliokuwa wakifanya kazi kwenye shamba hilo . Baada ya kuwa ameaga nyumbani kwake marehemu huyo alipakia chakula hicho kwenye pikipiki yake na kuelekea kwenye shamba hi...
Karibu kwenye Blog Yetu na tupo tayari kukuhabarisha kwa Habari na Matukio mbalimbali kwa Weledi Masaa 24 popote ulipo,kama una taarifa au unataka kutangaza na Sisi tafadhali wasiliana nasi kupitia ukurasa huu. Pia tunapatikana YouTube @sitetvtz,Instagram,Twitter na Facebook @sitetvtz. Ofisi zetu zipo Jengo la Mpanda Plaza Ghorofa ya 3,Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi.